• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

PAMS FOUNDATION YAPONGEZWA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Posted on: July 19th, 2025

Taasisi isiyo ya kiserikali ya PAMS Foundation imepongezwa kwa mchango wake mkubwa katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi wa maeneo ya vijijini kwa kuwapatia mitungi ya gesi bila gharama yoyote, hatua inayosaidia kuhifadhi mazingira na kuboresha afya za watumiaji.


Pongezi hizo zimetolewa Julai 19, 2025 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa wakati akizungumza na wananchi wa kijiji Cha Digoma na Maskati kwenye ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa misitu unaotekelezwa na Taasisi hiyo.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Katibu Tawala huyo amesema juhudi za PAMS Foundation zinachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza utegemezi wa matumizi ya kuni na mkaa kama chanzo kikuu cha nishati, hatua inayosaidia pia kupunguza uharibifu wa misitu.


“...tena niwasifu sana na ukweli mmekuwa mkishirikiana sana Serikali hasa kile kitendo mnachofanya cha kuwapa hawa wananchi gesi ili tupunguza ya kuni...huu mpango naomba uendelee...amesema Katibu Tawala.


Aidha, ameongeza kuwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kinala barani Afrika katika kuhakikisha kuwa wananchi wanatumia nishati safi na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa huku akiongeza kuwa nchi inamalengo ya kufikia asilimia 80 mwaka 2030 wananchi wawe wanatumia nishati safi.


Sambamba na hilo, Dkt. Mussa amesema Mkoa wa Morogoro utaendelea kutafuta wadau mbalimbali wa maendeleo ili kuhakikisha kuwa asilimia 80 ya lengo inafikiwa.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Ndg. Paulo Faty amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa kwa kukagua utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa misitu katika Wilaya hiyo.


Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi kutoka PAMS Foundation, amesema kuwa ugawaji wa mitungi hiyo ya gesi ni sehemu ya kutoa hamasa kwa wananchi ambao wamejiunga katika mradi huo. Aidha, amebainisha kuwa katika kijiji cha Maskati wamepata eneo la kutekeleza miradi huo lenye ekari 250 ambapo zoezi la upimaji linaendelea.


Nao baadhi ya Wananchi wa Vijiji hivyo wameonesha kufurahishwa kwao na uwepo wa mradi huo ambao utawasaidia kurudisha uoto wa asili na kuwawezesha kupata kipato

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MZUMBE UNIVERSITY YAUNGA MKONO KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID, YAKABIDHI VITABU 400 VYA SHERIA

    July 21, 2025
  • PAMS FOUNDATION YAPONGEZWA KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

    July 19, 2025
  • RAS MOROGORO ARIDHISHWA NA MRADI WA UBORESHAJI MISITU, AMUAGIZA DED MVOMERO KUSHUGHULIKIA SUALA LA HATI

    July 17, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUTOGOMEA MIRADI YENYE TIJA KWENYE UCHUMI

    July 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.