• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

NFRA YASHUSHA NEEMA KWA WAKULIMA WA NAFAKA MVOMERO

Posted on: July 15th, 2023

Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) wametangaza rasmi kuanza kununua mazao kupitia vituo vyake vilivyopo katika maeneo mbalimbali Tanzania nzima, fursa ambayo Wanamvomero kwa kipindi kirefu wamekuwa wakiililia.

Akiongea mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Bungoma, Kata ya Mkindo Wilayani Mvomero, Mwakilishi wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula,NFRA kanda ya kipawa Ndg. Mgeni Mussa amesema kuwa kwa kipindi kirefu wamekuwa wakiwafikia wakulima wa nafaka maeneo mbalimbali nchini na sasa neema hii imewafikia  wakulima wa Mvomero.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli akizindua mwongozo wa ununuzi wa mazao ya wakulima kwa wafanyabiashara, amewataka wafanyabiashara wazingatie mpango huo ili Serikali na Halmashauri ziweze kukusanya ushuru ili Serikali itoe huduma za msingi kwa wananchi wake.

“Tunaomba wanunuzi wa mazao wapitie Halmashauri wapewe vibali vya ununuzi wa mazao. Serikali ya awamu ya sita ina nia ya kulinda maslahi ya wakulima.Tuzalishe mazao ya kutosha, shule nyingi za Mvomero pia zinahitaji chakula.” Amesema Mkuu wa Wilaya hiyo wakati akiongea na Wananchi wa Kijiji cha Bungoma.

Kuhusu fursa iliyoletwa na Wakala wa hifadhi ya Chakula (NFRA) Mkuu wa Wilaya amewaasa wakulima wa Mvomero kuitumia fursa hiyo vizuri kwani bei ya ununuzi inayotolewa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula ni bora kuliko ile inayotolewa na wafanyabiashara walanguzi wasiozingatia maslahi ya Wakulima.

“Zali limetuangukia Wanamvomero, naomba tutumie fursa hii na pia tulinde amani yetu. Wanunuzi wamekuja hapa kwa kuwa kuna amani.” Aliongeza Mkuu wa Wilaya.

Kwa upande wake Meneja  wa kanda ya Kipawa Ndg. Mgeni Mussa amewahakikishia wakulima uhakika wa malipo yao mara tu baada ya mauzo. “Malipo ni ndani ya masaa 24. Kama ukikamilisha kila kitu, mara baada tu ya mauzo, pesa yako unaipata kesho yake.”

Kata ya Mkindo ni moja ya Kata zinazozalisha mpunga kwa wingi sana kwa Mkoa wa Morogoro. Serikali ya awamu ya sita imewekeza Bilioni 5.6 kuanzia Septemba mwaka 2022 kwa mradi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Mgongola ambayo itawahakikishia wakulima uhakika wa kulima mazao mwaka mzima.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.