• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MZUMBE UNIVERSITY YAUNGA MKONO KAMPENI YA MAMA SAMIA LEGAL AID, YAKABIDHI VITABU 400 VYA SHERIA

Posted on: July 21st, 2025

Chuo Kikuu cha Mzumbe kimeonyesha mshikamano na Serikali katika kukuza upatikanaji wa haki kwa wananchi kwa kukabidhi vitabu 400 vya sheria kwa ajili ya kuunga mkono Kampeni ya Mama Samia Legal Aid Wilayani Mvomero.


Makabidhiano hayo yamefanyika Julai 21, 2025 katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ambapo kitabu hicho kinaitwa Utekelezaji wa Sheria, kitatumika kutoa msaada wa kisheria kwa viongozi wa Serikali za Vijiji katika Wilaya hiyo.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg. Paulo Faty ameushukuru uongozi wa chuo hicho kwa kuona umuhimu wa kutoa msaada wa kisheria kwa viongozi wa ngazi ya chini ambao muda mwingi wanakaa na wananchi na hata maamuzi ya kisheria uanzia kwao.


Aidha, Mkurugenzi Mtendaji huyo amebainisha kuwa utoaji wa vitabu hivyo ni sehemu ya kuunga mkono Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid) ambapo Viongozi pamoja na wananchi watanufaika na uwepo wa vitabu hivyo.


Kwa upande wake, Afisa Maktaba kutoka Chuo Mzumbe Bi. Sarah Mwambalasa amesema wanakabidhi vitabu 400 vya utekelezaji wa sheria ambavyo vina thamani ya shilingi 4,000,000 vinatarajiwa kuwasaidia wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na wajumbe wa Serikali ya Vijiji.


Naye, Mhadhiri Msaidi Kitivo cha Sheria Bw. Hamisi Yange kutoka Chuo hicho amesema vitabu hivyo vimeandikwa na waandishi wawili, pia vinatoa muongozo wa kutambua na kufahamu Sheria mbalimbali zilizopo hapa nchini huku akibainisha kuwa kina sura 16.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.