• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MWENYEKITI WA KIJIJI CHA LUKENGE AFARIKI DUNIA KWA KUSHAMBULIWA NA MAMBA, DC NGULI ATOA AGIZO KWA TAWA

Posted on: January 21st, 2025

Katika tukio la kushtua wakazi wa kijiji cha Lukenge wilayani Mvomero, Mwenyekiti wa kijiji hicho, Bw. Anselem John, anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 60 amefariki dunia baada ya kushambuliwa na mamba wakati akinawa maji kwenye mto Mkindo uliopo kando na shamba lake.

Kwa mujibu wa taarifa za mashuhuda, wamesema tukio hilo limetokea januari 21, mwaka huu ambapo marehemu alikuwa akinawa maji baada ya kukamilisha shughuli zake za kilimo ndipo huo aliposhambuliwa na mamba na kupelekea kifo chake. Mwili wa marehemu ulipatikana alfajiri ya Januari 22, 2025 kwenye kingo za mto huo ukiwa na majeraha makubwa.

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Judith Nguli, amefika katika eneo la tukio na kutoa pole kwa familia ya marehemu na wakazi wa kijiji hicho. Akizungumza na wanakijiji, Mhe. Nguli ametoa agizo kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kushughulikia mamba walioko kwenye mto huo haraka iwezekanavyo.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amesema kupitia taarifa ya wanakijiji zaidi ya watu 17 wamepoteza maisha kutokana na mamba lakini wananchi hawakuwahi kuripoti sehemu yoyote hivyo, ameitaka TAWA kuhakikisha wanadhibiti mamba hao ili kuepusha kutokea kwa vifo zaidi vinavyotokana na mashambulizi ya mamba.

Mhe. Nguli amebainisha jitihada ambazo Serikali itachukua kwa haraka ikiwemo kurekebisha pampu ya kisima cha maji katika kijiji hicho ili wananchi waache kwenda mtoni na badala yake watumie maji ya kisima hiko.

Naye, Afisa wa wanyamapori kutoka TAWA Bw. Paul Mbeya amesema kuwa taasisi hiyo inaendesha zoezi la uvunaji wa mamba ambalo lilianza tangu mwaka 2024, huku akiongeza kuwa kupitia agizo la Mkuu wa Wilaya wanaanza zoezi la kusaka mamba hatarishi katika mto huo  na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano ili kufanikisha jambo hilo.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.