• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Wilaya Akagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi

Posted on: November 6th, 2018

Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa Wilaya Ndugu Maneno Chisepo akiambatana na wajumbe wa kamati hiyo,hivi karibuni walitembelea na kukagua Miradi ya Maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 katika Halmashauri .

Jumla ya miradi ya maendeleo kumi na sita (16) ilitembelewa na kukaguliwa na kamati hiyo  ambayo ni; Mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Pemba ambapo upo katika hatua ya lenter, ukarabati na ujenzi wa kituo cha afya Kibati, mradi wa maji wa Hoza /Salawe, Zahanati ya Difinga, mnada wa Mziha, mradi wa Skimu ya umwagiliaji Lukenge, Soko la mazao Madizini, kuweka mashine na ghala kijiji cha Bungoma kata ya  Mkindo kupitia mradi wa PHRD, Skimu ya umwagiliaji Msufini, Zahanati Lukunguni Kata ya Kikeo, Shule ya Msingi Kododo Kata ya Luale, Shule ya msingi Kibuko Kata ya Nyandira ujenzi wa matundu ya vyoo, machinjio Changarawe Kata ya Mzumbe, Soko la mazao Tangeni Kata ya Mzumbe, Mradi wa barabara ya Langali - Nyandira urefu wa Km. 5.2,

Hii ni Shule ya Msingi Pemba yenye jumla ya wanafunzi 982, wavulana 486, wasichana 496 na walimu 11, walimu  wanaume 9 na walimu wanawake 2.

Hali ya miundombinu katika Shule ya Msingi Pemba haitoshelezi kulingana na mahitaji yaliyopo; matundu ya vyoo na nyumba za walimu hazitoshelezi kulingana na mahitaji ya Shule. Shule inahitaji madarasa 21, yaliyopo kwa sasa ni 4, pungufu ni 17. Wananchi wa Pemba walianzisha ujenzi wa vyumba 3 vya madarasa kwa kuchangishana hadi kufikia hatua ya boma ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika madarasa machache waliyonayo kwa sasa.

Ujenzi wa maboma haya umegharimu kiasi cha Shilingi milioni sita na laki tano (6,500,000/=) ambapo Mfuko wa jimbo ulichangia Tshs. 2,000,000/=na nguvu za wananchi ni Tshs. 4,500,000/=

Ili kukamilisha ujenzi wa maboma hayo inahitajika jumla ya Tshs. 15,890,000/=. Serikali ya Kijiji cha Pemba imewasilisha maombi ya fedha kwa Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo, maombi hayo yakiwa nje ya mpango wa bajeti wa mwaka  fedha 2018/2019.

Mwenyekiti  wa Kamati ya Siasa ya Wilaya Mvomero baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mvomero Ndugu Florent Laurent Kyombo,  walikagua ujenzi huo wa vyumba vya madarasa na kuwapongeza wanakijiji na walimu kwa kazi nzuri ya ujenzi wa maboma hayo ya madarasa, pia walimuagiza Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha wanapata fedha katika vyanzo vya ndani ili kumalizia majengo hayo na ifikapo Januari 2019, yaanze kutumika.


Wajumbe wa Kamati Ya Siasa wakikagua boma

Kamati ya Siasa ikifanya ukaguzi wa Boma

Mkurugenzi Mtendaji (wa Pili kutoka kushoto) Akisoma taarifa ya utekelezaji wa Mradi

 wa Ujenzi wa Maboma ya vyumba viwili vya Madarasa katika shule ya Msingi Pemba,

iliyopo kata ya Pemba.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.