• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MVOMERO YAAZIMIA KUPELEKA ANDIKO SERIKALINI KUOMBA KUONGEZEWA BAJETI YA TARURA

Posted on: February 18th, 2025

Wilaya ya Mvomero imeazimia kuwasilisha andiko maalum serikalini ili kuomba kuongezewa bajeti kwa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara katika wilaya hiyo.

Azimio hilo limefikiwa leo Februari 18, 2025 katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) kilicholenga kupitia na kujadili mapendekezo ya mpango wa bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.

Aidha, wajumbe wa kikao hicho wamejadili changamoto kubwa ya ubovu wa barabara zinazosimamiwa na TARURA, hali inayosababisha usumbufu kwa wakazi na wafanyabiashara katika shughuli zao za kila siku.

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amesema hali ya uzalishaji katika Wilaya hiyo ni mkubwa lakini miundombinu ya barabara sio rafiki, hata hivyo amesema kuwa kuna wakati TARURA inashindwa kutekeleza miradi yake kutokana na bajeti kuwa ndogo, hivyo kuna haja kama Wilaya kuisaidia TARURA ili iongezewe bajeti.

"...ili tuwasaidie lazima tutoke na maazimio ya hali halisi ya barabara zetu hapa ili tupeleke juu kwa ajili ya msaada waongezewe bajeti..." amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Judith Nguli ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwa kuandaa mpango wa bajeti ambayo itaenda kuivusha Halmashauri hiyo, huku akimshauri Afisa Mipango wa Halmashauri kuongeza vyanzo vingine vya mapato vikiwemo ushuru wa viwanja, Vibali vya ujenzi pamoja na hoteli, nyumba za wageni, vituo vya mafuta na mashine za mbao.

Akiwasilisha mapendekezo ya mpango na bajeti ya mapato  na matumizi kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Amos Kanige amesema kuwa Halmashauri inakisia kukusanya jumla ya shilingi Bilioni 59,976 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri, Ruzuku ya Serikali kuu na wadau wa maendeleo.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa TARURA Wilaya ya Mvomero Mhandisi Said amesema kuwa mpango wa bajeti ya matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2025/2026 TARURA inatajaria kutumia shilingi Bilioni 3,943.762 kwa ajili ya matengenezo ya barabara.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.