• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MVOMERO YAANZA UTEKELEZAJI KAMPENI YA TUTUNZANE

Posted on: August 15th, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli leo Agosti 15, 2024 ameongoza kikao cha wadau wa Sekta za Kilimo na mifugo kwa lengo la kuhamasisha urasimishaji wa Ardhi kwa wakulima na wafugaji kuelekea utekelezaji wa Kampeni ya Tutunzane Mvomero 2023 – 2028 ambayo ilizinduliwa Agosti 3, 2024 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhe. Nguli amesema zoezi lililopo kwa sasa ni kuhamasisha wakulima na wafugaji kurasimisha ardhi zao ili waweze kupatiwa hati miliki za mashamba hayo na hatimae wapatiwe mbegu za malisho na ufuta kwa ajili ya kupanda.

“…leo nina mkutano huu wa kuhamasisha urasimishaji wa ardhi kwa wakulima na wafugaji, mwenye eneo akamilikishwe kihalali, apate hati yake, apate malisho yake, achimbe kisima chake ili aweze kuondokana na haya maugomvi ambayo yanatuharibia Amani ya nchi yetu…” amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, amesema kwa niaba ya Serikali atawasaidia wakulima na wafugaji kumili ardhi huku akibainisha kuwa Serikali itatoa wataalam wa kilimo na mifugo ili waweze kuwahudumia kwa karibu kipindi chote cha kilimo cha malisho na ufuta.

Sambamba na hilo, Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wakulima na wafugaji kutumia fursa ya uwepo kampeni ya TUTUNZANE MVOMERO kupima maeneo yao kwa kuwa zoezi hilo hutumia gharama ndogo ukilinganisha na upimaji wa ardhi nje ya kampeni hiyo.

Naye, Afisa Mifugo Mwandamizi Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Onesmo Ngenzi amesema lengo la Kampeni hiyo ni kuwamilikisha Ardhi wafugaji hivyo hawana budi kununua ardhi ya kutosha, ameongeza kuwa Wizara itahakikisha wafugaji na wakulima wanapata mbegu ili waweze kuzipanda katika mashamba yao.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Morogoro Bw. Julius Mwakafwila amebainisha kuwa kwa mujibu wa Sheria za Ardhi kuna aina Tatu za Ardhi ambazo ni Ardhi ya Kijiji, Ardhi ya Jumla (kawaida) na Ardhi ya Hifadhi. Pia amesema wakati wa zoezi la upimaji wa ardhi kutakuwa na uzingatiaji wa aina za ardhi zilizobainishwa.


MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.