• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MVOMERO, TMDA WAONDOSHA DAWA ZILIZOINGIZWA NCHINI KINYUME NA TARATIBU

Posted on: February 15th, 2025

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kwa kushirikiana na Wilaya ya Mvomero imefanikiwa kuondosha dawa zilizoingizwa nchini kinyume na taratibu katika operesheni maalum ya kudhibiti usambazaji wa dawa haramu na zisizo salama kwa matumizi ya binadamu.

Operesheni hiyo, iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, ilibaini uwepo wa dawa ambazo ziliingizwa bila kufuata sheria na bila kibali cha TMDA zilitolewa na mfadhili kwa ajili ya zahanati katika kijiji cha Mela, Kata ya Mangae, hali inayohatarisha afya za wananchi.

Akizungumza Februari 15, 2025 kwenye mkutano na wananchi wa kijiji cha Mela Afisa wa TMDA Bi. Riziki Shemula ameeleza kuwa baada ya kupata taarifa ya uwepo wa dawa hizo amefanya ugakuzi ambapo imebainika kuwa dawa hizo hazitambuliki na Serikali kwakua hazijasajiliwa na mamlaka husika, mfadhili huyo hakuwa na kibali cha kuingiza dawa nchini.

Aidha, ukaguzi huo pia umebaini kuwa uhifadhi wa dawa hizo haukufuata taratibu maalum za kuhifadhi dawa, pia dawa hizo muda wake wa matumizi umeisha.

Kufuatia maelezo ya Afisa wa TMDA, Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli ametoa maelekezo kwa niaba ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya akiwataka wafadhili wanaojitolea kuleta misaada kwa wananchi wa Wilaya hiyo wafuate sheria, taratibu na miongozo ya nchi. Aidha, ameongeza kuwa dawa hizo zinatakiwa kuteketezwa kwakua si salama tena.

Sambamba na hilo, Mhe. Judith Nguli amemuagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa zahanati hiyo inaanza kutoa huduma kwa wananchi wa eneo hilo.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mangae Mhe. Christopher Maarifa amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa maelekezo aliyoyatoa na kuhaidi kuyafanyia kazi.

Nao baadhi ya wananchi wa Kijiji hicho wameishukuru Serikali kwa hatua hiyo na kwamba inajali Afya za wananchi wake.

Dawa hizo zina uzito wa kilo 150 na zinathamani  ya shilingi 43, 126, 517/=

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • RAS MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA "JISOMESHE NA MKARAFUU" KUWAWEZESHA WANAFUNZI KIUCHUMI

    March 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.