• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MVOMERO KUUZA UFUTA KUPITIA STAKABADHI GHALANI KUANZIA MEI 20, 2025

Posted on: May 16th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imetangaza rasmi kuanza kwa mauzo ya zao la ufuta kupitia mfumo wa Stakabadhi Ghalani kuanzia Mei 20, 2025, hatua inayolenga kuhakikisha wakulima wananufaika kwa kupata bei nzuri ya mazao yao.

Hayo yamebainishwa Mei 16, 2025 na Katibu Tawala Wilaya ya Mvomero Ndg. Said Nguya wakati wa kikao cha Wadau wa Stakabadhi za Ghala kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo wajumbe wa kikao hicho wameunga mkono azimio hilo.

Katibu Tawala huyo amewataka Waheshimiwa Madiwani, Watendaji wa Kata na Vijiji, Maafisa Ushirika na Maafisa Ugani pamoja na wataalam wa kilimo kushirikiana kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa Mfumo huo na kuwahamasisha kuutumia ili waweze kupata faida ambayo wamekusudia kuipata.

"...kwa hiyo kikao hiki tunakubaliana kwamba zao la ufuta kwenye stakabadhi ya ghala tunaanza rasmi tarehe 20 mwezi wa tano..." amesema Ndg. Said Nguya.

Aidha, pamoja na azimio hilo wajumbe wa kikao hicho wameadhimia kuongeza vituo vya ukusanyaji wa mazao katika maeneo ambayo yanachangamoto ya maghala ili kudhibiti walanguzi wa mazao ya wakulima.

Sambamba na hilo, Wajumbe wameazimia kuwa Maafisa Ushirika wahamasishe wakulima kujiunga katika vyama vya Ushirika katika Tarafa za Mlali na Mgeta.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Bi. Loema Peter amewataka Maafisa Ushirika, Maafisa ugani, kilimo pamoja na watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha kuwa wanafanikisha suala hilo huku akiwataka kila mmoja kuwajibika katika nafasi zao.

Ameongeza kuwa hadi kufikia siku ya jumatatu maandalizi muhimu yatakuwa yamekamilika huku akisema kuwa wananchi watapatiwa elimu ili wawe na uelewa na mfumo huo.


Akielezea mikakati ya Halmashauri katika kuongeza uzalishaji wa zao la kakao, Afisa Ushirika wa Halmashauri hiyo Bw. Mihayo Lukaya amesema kuwa Halmashauri imeweka mikakati ya kuanzisha kitalu cha miche ya kakao 100,000 kila mwaka, ambapo hadi sasa miche 12, 254 imezalishwa na kugawanywa bure kwa wakulima wa Kata za Mhonda, Kweuma, Sungaji, Diongoya na Maskati.


MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WITO UMETOLEWA KWA WADAU, SERIKALI KUONGEZA JUHUDI KATIKA UTOAJI ELIMU YA HEDHI SALAMA VIJIJINI

    May 28, 2025
  • WAHE. MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA WATEMBELEA MVOMERO KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI UNAVYOWAKOMBOA WAKULIMA WA KAKAO

    May 24, 2025
  • MVOMERO KUUZA UFUTA KUPITIA STAKABADHI GHALANI KUANZIA MEI 20, 2025

    May 16, 2025
  • MKURUGENZI INEC AWASISITIZA WAANDHISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NGAZI YA KITUO KUZINGATIA MUDA WA KUFUNGUA VITUO VYA KUANDIKISHA WAPIGA KURA

    May 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.