Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imejipanga kuendelea kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo mbalimbali ikiwemo vituo vya kutolea huduma za Afya ambavyo vinamfumo wa GoT-HoMIS (Government of Tanzania Health Operation Management Information System).
Hayo yamesemwa Mei 9, 2025 na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bi. Mary Kayowa wakati akizungumza na watumishi wa Idara ya Afya kwenye kikao cha tathmini ya utendaji kazi wa vituo vya kutolea huduma za afya kwa robo ya tatu (Januari – Machi) kilichpfanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.
“...tutajikita sana kwenye suala zima la ukusanyaji wa mapato kupitia hii GoT-HoMIS...” amesisitiza Kaimu Mkurugenzi.
Aidha, Bi. Mary amewataka wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya kuongeza ufanisi kwenye matumizi ya mfumo huo huku akimuelekeza Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kuwasilisha taarifa ya vituo ambavyo bado havijaanza kutumia mfumo huo katika vituo vyao.
Katika hatua nyingine, Kaimu Mkurugenzi huyo amewasisitiza wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya kuhakikisha kwa wanasimamia miradi ya afya inayotekelezwa katika Vituo vyao kwa kuzingatia ubora na thamani ya fedha iliyotolewa (Value of Money).
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Dkt. Philllipina Phillipo amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kutathmini hali ya utoaji wa huduma za Afya kwa robo ya tatu (Januari - Machi). Aidha, amemshukuru Kaimu Mkurugenzi kwa hotuba yake huku akiahidi kuyafanyia kazi maelekezo aliyoyatoa.
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.