• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MMILIKI WA KITUO CHA MAFUTA MZIHA APEWA SIKU MOJA KUWASILISHA TAARIFA ZA MIKATABA.

Posted on: April 20th, 2024

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 Ndg. Godfrey Eliakimu Mzava amemtaka mmiliki wa kituo cha mafuta cha Matemba kilichopo katika kijiji cha Mziha Wilayani Mvomero kuwasilisha kwa kiongozi huyo taarifa za mikataba ya wafanyakazi wa kituo hicho

Ndg. Godfrey Mzava ametoa agizo hilo Aprili 20 mwaka huu wakati akizindua mradi wa kituo cha Mafuta kilichopo Kijiji cha Mziha Wilayani Mvomero, Mkoani Morogoro.

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 amesema kuwa wafanyakazi wa kituo hicho hawana mikataba rasmi hivyo amemuagiza Mmiliki wa kituo hicho akisimamiwa na Mwanasheria wa Halmashauri ya Mvomero kuhakikisha wafanyakazi hao wanapatiwa mikataba na kuwasilisha taarifa za mikataba hiyo kwa kiongozi huyo.

"...namuelekeza Mwanasheria wa Halmashauri leo hii awasimamie na kuandaa huo mkataba...baada ya kila mtumishi apate mkataba..."amesema Ndg. Godfrey Mzava.

Katika hatua nyingine, Kiongozi huyo amewataka wataalam wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kufunga vifaa vya kutambua viashiria vya uwepo wa moto katika kituo hicho ndani ya siku tatu kuanzia leo Aprili 20, 2024 mafuta ili kusaidia kupunguza hatari ya kutokea kwa moto kituoni hapo.

Awali wakati akisoma taarifa ya ujenzi wa kituo hicho Bw. Peter Mamilo amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Disemba 2023 na kukamilika Machi 2024 huku akibainisha kuwa mradi umegharimu zaidi ya milioni 300 hata hivyo umeshakamilika kwa asilimia 100 na umeanza kutoa huduma kwa wananchi. Pia ameongeza kuwa mradi huo utawasaidia wakazi wa Mziha na maeneo jirani kuwapunguzia adha ya kutembea zaidi ya kilometa 35 kufuata huduma ya mafuta maeneo mengine.

Mwenge wa Uhuru 2024 umepokelewa katika kijiji cha Mziha leo Aprili 20 na kuanza kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero huku ukiambatana na Kaulimbiu isemayo Tunza Mazingira na shiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa maendeleo endelevu.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.