• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA YA MVOMERO AJITAMBULISHA NA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI KATA YA KANGA

Posted on: October 9th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Maulid Dotto ameendelea na ziara yake ya kujitambulisha, kujua maeneo ya mipaka na kusikiliza kero za wananchi katika Kata na Vijiji vya Wilaya ya Mvomero, ambapo Oktoba 9, 2025 amefika Kijiji cha Kanga na Dihinda Kata ya Kanga akiwa ameambatana na Wataalam kutoka Halmashauri na Taasisi mbalimbali zilizomo ndani ya Wilaya ya Mvomero.

Katika mkutano huo wa hadhara, wananchi walipata fursa ya kueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo tatizo la umeme hususan Kitongoji cha Kisauke, wafugaji kuingiza ng'ombe kwenye mashamba ya wakulima, ubovu wa barabara, mpaka wa hifadhi usogezwe ili wananchi wapate maeneo ya kuishi, ndege aina ya quelequelea wanakula mazao ya mpunga, barabara inayounganisha mikoa ya Pwani na Tanga itengenezwe, wanafunzi wanatembea umbali mrefu Km 4 kutoka Shule mama ya Kanga wananchi wanaomba wajengewe Shule ya mkondo, utoaji wa hati miliki za ardhi utekelezaji wake haufiki mwisho, pembejeoza kilimo zinapatikana mbali Madizini mjumbe aliomba huduma zisogezwe na mwananchi alilalamikia eneo la shamba lake kuvamiwa na mwekezaji hata akikodisha anakuja kumtishia.


Akizungumza baada ya kusikiliza kero hizo, Mhe. Dotto aliwataka Wataalam watoe majibu kwa hoja zilizowasilishwa mezani pia aliawahakikishia wananchi kuwa Serikali ya Wilaya ya Mvomero imedhamiria kusikiliza na kushughulikia kero zote kwa wakati ili kuhakikisha amani, utulivu na maendeleo vinaendelea kupatikana katika maeneo yote ya Wilaya. Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Viongozi wa Vijiji na wananchi katika kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi.

Aidha alisisitiza kuwa Serikali ina dhamira ya dhati ya kuboresha maisha ya wananchi wa Mvomero kupitia utatuzi wa migogoro, uboreshaji wa miundombinu na upanuzi wa huduma za jamii.

Wananchi walimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kufika kusikiliza kero zao moja kwa moja na kuonesha matumaini kuwa hatua stahiki zitachukuliwa ili kupunguza changamoto wanazokabiliana nazo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MKUTANO WA BARAZA LA KATA ROBO YA PILI OKTOBA - DISEMBA 2025/2026

    January 29, 2026
  • FURSA ZA UWEKEZAJI ISIWE CHANZO CHA MIGOGORO YA MIPAKA YA VIJIJI, VIONGOZI WATAKIWA KUSIMAMA IMARA KUIMALIZA

    January 28, 2026
  • MIPANGO, BAJETI ZA HALMASHAURI ZIENDANE NA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050 - RC MALIMA

    January 27, 2026
  • DC MVOMERO ALIPONGEZA SHIRIKA LA SAWA KUJENGA MADARASA YA SHULE SHIKIZI, AAGIZA MCHAKATO WA USAJILI UANZE MARA MOJA

    January 23, 2026
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.