• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA : WATOTO WARIPOTI SHULE NDANI YA WIKI MOJA

Posted on: January 10th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli ametoa maelekezo kwa wazazi na walezi ndani ya Wilaya ya Mvomero kuhakikisha wanawaleta Watoto wao kuripoti shuleni ndani ya wiki moja kuanzia leo ikiwa ni siku 3 tu toka muhula mpya wa shule ufunguliwe kwa shule za awali msingi na sekondari kwa mwaka 2024 nchini Tanzania.

Mkuu wa Wilaya ametoa rai hiyo wakati alipofika kufanya tathmini ya uandikishaji wa wanafunzi wa darasa ya awali na Shule za Msingi pamoja na kuripoti kwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza mwaka 2024.

Katika ukaguzi wake alipopita katika Shule ya Msingi Kwamuhuzi, ameridhika na kasi ya uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali Pamoja na darasa la kwanza huku kwa darasa la kwanza uandikishaji ukiwa umefikia asilimia 83 huku bado wazazi wakihamasika kuandikisha Watoto wao na kuleta matumaini ya kufikia lengo la asilimia 100.

Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa wazazi kuwaandikisha Watoto wao na kutoa maelekezo kwa walimu wa shule hiyo kupokea wanafunzi wapya hata kama hawana sare za shule ili kuwaapa wazazi muda wa kutafuta sare hizo.

Aidha, katika ukaguzi wake kwa Shule ya Sekondari Kumbukumbu ya Sokoine, Mkuu wa Wilaya hajaridhishwa na kasi ya kuripoti kwa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza kwani kati ya wanafunzi 50 waliopangiwa kuanza kidato cha kwanza shuleni hapo, ni wanafunzi 16 tu ndio walioripoti na kuanza masomo.

Ametoa maelekezo kwa wazazi, walezi, watendaji wa kata na vijiji kuhamasisha na kufichua wanafunziwanaofichwa katika maeneo yao kuripoti shuleni na kuanza masomo kwani elimu ni haki na sio hisani na Watoto wanatakiwa kupata elimu kadri inavyotakiwa na kumchelewesha mwanafunzi masomo ni  kumnyima haki yake ya msingi.

Amesema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshafanya jukumu lake kuleta fedha kujenga miundombinu wezeshi Pamoja na kuondoa ada ili wanafunzi hao wasome, sasa ni jukumu la wazazi kuwapeleka Watoto waanze shule. Mkuu wa Wilaya amesema hatakuwa tayari kuona Watoto wanapoteza haki hiyo ya msingi.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.