• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA ATOA SIKU 3 MKANDARASI KULIPA DENI LA MILIONI 46.

Posted on: June 30th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amemtaka aliyekuwa Mkandarasi wa ujenzi wa kisima cha maji katika kitongoji cha Sokoine Ranchi kulipa madeni yake zaidi ya shilingi milioni 46 anayodaiwa na vibarua wake, mama lishe pamoja na mzabuni.

Mhe. Nguli ametoa agizo hilo Juni 28, mwaka huu wakati akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Sokoine Ranchi alipokwenda baada ya kupokea malalamiko ya wananchi juu ya Mkandarasi huyo.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema Mkandarasi uyo anatoka kwenye kampuni Selflink limited ambaye inasemekana ni mtumishi wa TANROADS  Rukwa. Kwa mujibu wa mkataba Mkandarasi huyo ameshalipwa asilima 90 ya kazi lakini kwa sasa amesimamishwa kuendelea na ujenzi huo.

Aidha, Mhe. Nguli amebainisha kuwa jitihada mbalimbali za kumtafuta zimefanyika ili alipe madeni yake lakini mkandarasi huyo hajajitokeza.

"...nimpe siku tatu huyo msimamizi wa mradi na kampuni yake siku tatu kuyalipa madeni yake mara moja..." amesema Mkuu wa Wilaya.

Sambamba na hilo Mhe Judith Nguli amewataka wananchi kurudisha mali za  mkandarasi walizochukua ikiwemo vifaa vya mradi pamoja na gari aina ya Toyota  Nissan lenye namba za usajiri T 471 AMK na kuwataka kutojichukulia sheria mkononi.

Kwa upande wao vibarua wanaomdai mkandarasi huyo akiwemo Bw. Juma Daniel amesema alipewa kazi ya kuchimba karo la tenki la maji ambapo  malipo yake ni shilingi 290,000 lakini hadi sasa amelipwa shilingi 150,000 tu.

Naye Bi. Halima Seluhinga amesema aliwapangisha chumba kwenye nyumba ya wageni ambapo pesa anayodai ni shilingi 500,000, flemu ya duka 70,000 na baadhi ya vyombo vimechukuliwa na wafanyakazi wa mkandarasi huyo. Aidha,  amebainisha kuwa aliamua kulizuia gari la mkandarasi hadi pale atakapolipwa lakini kwa maelekezo ya Mkuu wa Wilaya anarudisha gari hilo.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.