• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA ATOA AGIZO KWA UONGOZI WA KATA YA MLALI KUUNDA CHOMBO CHA WATUMIAJI MAJI NDANI YA JAMII

Posted on: August 20th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh.Halima Okash ameuagiza uogozi wa Serikali ya Kata ya Mlali kuhakikisha ndani ya siku 7 wawe wameunda Chombo cha  ya Watumia Maji ndani ya jamii ili kumaliza kero ya maji katika Kata hiyo.

Agizo hilo la Mkuu wa Wilaya amelitoa hapo jana katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo, mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Meneja wa RUWASA wa wilaya hiyo ya kuwa miongoni mwa sababu zinazosababisha ukosefu wa maji ni baadhi ya vijiji kushindwa kufanya uchaguzi kuwachagua wajumbe wa wawakilishi watakaounda Chombo cha watumia Maji katika kata hiyo jambo ambalo limesababisha migogoro ya mara kwa mara kati ya wananchi na viongozi wa serikali katika kata hiyo.

Mkuu huyo wa Wilaya amewataka viongozi wa serikali katika kata hiyo hususani wa Kijiji cha Mlali kusimamia vyema rasilimali za umma na kuwashirikisha wananchi katika masuala mbalimbali ya maendeleo ili kuleta utawala bora na uwajibikaji.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amesema ili maendeleo yaweze patikana ni lazima kuwepo na uwazi katika matumizi ya rasilimali za umma pamoja na ushirikishwaji wa wananchi katika utoaji maamuzi.

Katika hatua nyingine, Mh. Halima Okash amepiga marufuku shughuli zote za waganga wa jadi  maarufu kama Lambalamba (ramli chonganishi) kufanyika katika eneo lote ndani ya wilaya na atakayejihusisha na maswala hayo au kuwaleta waganga hao kwa ajili ya shughuli hizo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg. Hassani Njama amesema miongoni mwa mambo yanayorudisha nyuma maendeleo ya kata hiyo ni migogoro ya mara kwa mara kati ya viongozi na wananchi, hivyo ameutaka uongozi wa kata hiyo kujitathmini upya na kumaliza tofauti zilizomo miongoni mwao na kuanza kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuleta maendeleo katika kata hiyo.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mh. Yusuf Makunja, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kutoa maelekezo hayo kwa uongozi wa kata hiyo ili kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa eneo hilo zikiwemo za ukosefu wa maji, upungufu wa vyumba vya madarasa na kupata ufumbuzi wa kutafuta eneo la kudumu kwa ajili ya ujenzi wa soko katika kata hiyo.

Mh. Makunja amemuahidi Mkuu wa Wilaya kwamba yeye pamoja na Mkurugenzi, watasimamia yale yote yaliyoelekezwa na Mkuu huyo ili kuweza kumaliza tofauti zote zilizopo katika kata hiyo ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.