• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

JAMII YATAKIWA KUSHIKAMANA KUPINGA MILA ZINAZOATHIRI HAKI ZA MTOTO

Posted on: June 16th, 2025

Jamii imetakiwa kushikamana kwa pamoja katika kupinga na kutokomeza mila na desturi kandamizi zinazokiuka haki za mtoto, ikiwemo ukeketaji, ndoa za utotoni na ajira za watoto, ili kulinda ustawi wa watoto na kuhakikisha wanapata haki yao ya msingi ya kuishi, kupata elimu na malezi bora.

Wito huo umetolewa Juni 16, 2025 na Afisa Tawala Wilaya ya Mvomero Bw. Flezier Mang’ula akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo kwenye maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambayo kiwilaya yamefanyika katika viwanja vya shule ya Msingi Manyinga B.

Bw. Mang’ula amesema kuwa mila potofu zimeendelea kuwa chanzo kikuu cha ukiukwaji wa haki za watoto hasa wa kike, jambo ambalo linadumaza maendeleo ya watoto na jamii kwa ujumla.

“…kwahiyo ni vizuri tukaendelea kukemea mila ambayo inamdumaza mtoto” amesema Bw. Mang’ula.


Ameongeza kuwa ni muhimu kwa viongozi wa kijamii na wa kidini kushirikiana na serikali katika kutoa elimu ya haki za watoto na kupinga mila zote zinazowadhalilisha au kuwanyima fursa ya maendeleo.


Kwa upande wao Watoto kupitia risala iliyosomwa wamesema ripoti zinaonesha kuwa matukio ya unyanyasaji kwa Watoto vimeongezeka kutoka visa 12163 mwaka 2022 hadi 15301 mwaka 2023, ubakaji uliongezeka kutoka 6827 kwa mwaka 2022 hadi 8691 mwaka 2023. Ameongeza kuwa matukio ya ukatili kwa mkoa wa Morogoro yameongezeka hadi matukio 976 mwaka 2023.


Naye, mwanafunzi Jackline Eliabe kutoka shule ya Msingi Manyinga A amebainisha aina mbalimbali za ukatili kwa Watoto zikiwemo ukatili wa kijinsia, saikolojia na ukatili wa kimwili aina hizo za ukatili huleta athari za moja kwa moja katika maendeleo ya mtoto.


Siku ya mtoto wa Afrika huadhimishwa kila mwaka Juni 16 ambapo kwa mwaka huu yamepambwa na kaulimbiu isemayo “Haki za Mtoto; Tulikotoka, Tulipo na Tuendako.


MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.