• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MVOMERO YAPONGEZWA KUONESHA JUHUDI UFUATILIAJI MADENI YA MIKOPO YA VIKUNDI

Posted on: June 12th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imepongezwa kwa kuonesha juhudi katika kufuatilia marejesho ya mikopo iliyotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kupitia asilimia kumi ya mapato ya ndani.

Pongezi hizo zimetolewa Juni 12, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima kwenye kikao cha Baraza la Madiwani cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa Halmashauri ya Mvomero imeonesha juhudi kutokana na utaratibu mzuri wa kuwasiliana na vikundi vilivyokopeshwa, kufuatilia maendeleo yao na kuchukua hatua stahiki kwa vikundi vilivyoshindwa kurejesha mikopo kwa wakati.

"...niseme jambo moja na hili lazima niliseme, katika Halmashauri zote ninyi mmechukua hatua zinazoeleweka kuliko watu wengine wote...." amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, ameitaka Halmashauri kuendelea kufuatilia kwa karibu na kuwasilisha taarifa ya hatua iliyofikiwa katika ufuatiliaji huo. Hata hivyo, ametoa wiki mbili kwa Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya ya Mvomero, Bi. Sia Ngao kuandaa mkakati unaoonesha muelekeo wa malipo ya mikopo iliyotolewa kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na wenye ulemavu.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa maelekezo na maagizo aliyoyatoa yatafanyiwa kazi kwa wakati.

Awali, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe. Yusuph Makunja wakati akifungua kikao hicho amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha usimamizi wa mapato ya Wilaya ya Mvomero.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.