• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

UWEPO KAZINI, KUFIKA KWA WAKATI NA KUFANYA KAZI KWA BIDII NI MSINGI WA HUDUMA BORA

Posted on: June 5th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Bi. Loema Peter, amesema kuwa ili wananchi wapate huduma bora ni lazima suala la uwajibikaji litekelezwe kwa dhati, likijumuisha kufika kazini kwa wakati, kuwepo kazini na kufanya kazi kwa bidii.

Mkurugenzi huyo ameyasema hayo Juni 5, 2025 wakati akizungumza na watumishi wa Idara ya Afya kwenye kikao cha kupokea taarifa za maendeleo ya Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa Mwezi Mei, 2025, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Bi. Loema Peter ameeleza kuwa nidhamu ya muda na uwepo wa watumishi katika maeneo yao ya kazi ni misingi muhimu katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

“Ili huduma zitoletwe na ziwe ni huduma bora, suala la uwepo wetu kazini, kufika kwa wakati na kufanya kazi ni jambo muhimu sana,” amesema Bi. Loema Peter


Aidha, amewataka Wasimamizi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya katika Halmashauri hiyo kuhakikisha wanakuwa mfano wa kuigwa kwa kuzingatia maadili ya kazi na kuwasimamia ipasavyo watumishi walioko chini yao, ili kuhakikisha malengo ya Serikali katika kuwahudumia wananchi yanafikiwa.


Sambamba na hilo, amewataka kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora za Afya kwa wananchi huku akibainisha kuwa Serikali imeboresha miundombinu ya Afya kwa kujenga Hospitali, Vituo vya Afya pamoja na Zahanati huku ikiboresha na maslahi ya watumishi hivyo, ni wajibu wao kutoa huduma bora.


Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji huyo amewataka Wasimamizi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya kusimamia miradi ya afya inayotekelezwa katika maeneo yao na kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa kulingana na fedha iliyotolewa.


Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Phillipina Phillipo amesema kuwa Idara imeweka utaratibu wa kufanya vikao vya tathmini kwa kila mwezi ambapo kila msimamizi wa kituo cha Afya anawasilisha taarifa ya kituo chake.


Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya watumishi wa Afya Ndg. Lubadanja amemshukuru Mkurugenzi kwa maelekezo aliyatoa huku akiahidi kuwa wataenda kuyafanyia kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.