• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA ASISITIZA UMOJA KWA WATENDAJI WA SERIKALI

Posted on: December 20th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewaasa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kuwa na umoja katika utendaji kazi kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kuwatumikia wananchi na kusogeza maendeleo katika sehemu zao za kazi.

Mkuu wa Wilaya ameyasema hayo katika kikao-kazi cha ndani  alichofanya pamoja na Watendaji mbalimbali wa Serikali wakiwemo Watendaji wa Kata, Vijiji pamoja na Wenyeviti wa Serikali Vijiji wa Tarafa ya Mvomero kilichofanyika Makao Makuu ya Kata kijiji cha Mvomero Jumatano, 20 Desemba 2023.

Katika Kikao hiko , Mkuu wa Wilaya amewataka kuitumikia dhamana waliyopewa na Serikali kwa kusimama na kufanya kazi kwa pamoja na waache tabia ya baadhi yao kuleta mpasuko kwenye vijiji vyao na badala yake wasikilize na kutatua kero za wananchi kwani wananchi ndio waliowapa nafasi walizokuwa nazo hivi sasa.

Mkuu wa Wilaya amesema ya kwamba amegundua baadhi ya Wenyeviti wa Mitaa wameanza kampeni za chinichini kuwania nafasi za uongozi mapema sana kinyume na utaratibu uliowekwa na Serikali jambo ambalo linaleta mpasuko na kukwamisha baadhi ya shughuli za Serikali hivyo ni vyema wawe wapole kipindi hiki ili kuruhusu viongozi waliopo wamalize muda wao. “Serikali inapenda viongozi wanaoiunganisha Serikali na sio kuigawa, tofauti zetu zisiigawe Serikali”. Alisema Mkuu wa Wilaya.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya amewataka Watendaji hao kusimamia vizuri miradi ya Serikali iliyo katika maeneo yao ya kazi. Amewata viongozi hao kuhakikisha kwamba miradi yote inayoletwa na Seriikali inasimamiwa ipasavyo mpaka kukamilika kwake kwani Serikali inapeleka fedha sehemu nyingi sana kwa ajili ya miradi mbalimbali hivyo miradi hiyo kuletwa Mvomero ni nafasi ya kipekee.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya amesisitiza umihimu wa lishe mashuleni na kuwataka wazazi , walezi pamoja na jamii iahkikishe inachangia lishe mashuleni ili kukuza taifa lenye afya tele. Pia amekemea migogoro ya wakulima na wafugaji na kuwaomba viongozi hao waunge mkono kampeni ya kitaifa ya Tutunzane Mvomero 2023 inayoenda kuwa chachu za migogoro hii kwenye Wilaya ya Mvomero.

Mwisho kabisa Mkuu wa Wilaya amekemea tabia ya baadhi ya Watendaji wa Serikali kutembea na mihuri na kuwaomba wairudishe mihuri hiyo ofisi kwani ina nguvu kubwa na ikitumiwa vibaya ni chanzo cha migogoro ya ardhi.

Alisisitiza pia umuhimu wa watendaji wa Serikali kukaa kwenye vituo vyao vya kazi ili kuhudumia wananchi. Pia alisisitiza kuwa makini na suala la ugaidi pamoja na uvunjifu wa amani. “Ukiona sura ngeni, toa taarifa”

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.