• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA AAHIDI HAKI UTATUZI WA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Posted on: July 16th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya MVomero Mheshimiwa Judith Nguli amewaahidi Wananchi wa Mkindo kuwa kutakuwa na haki katika usuluhishi wa migogoro ya Wakulima na Wafugaji katika Kata ya Mkindo na maeneo mengine Wilayani Mvomero.

Mkuu wa Wilaya ametoa ahadi hiyo wakati alipofanya ziara kukagua Skimu ya Umwagiliaji ya Mgongola iliyopo Kata ya Mkinda Wilayani humo. Ameyasema hayo wakati akiongea na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Bungoma Wilayani Mkindo alipoenda kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili wananchi wa Mkindo Jumamosi tarehe 15, Julai 2023.

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amesema hafurahishwi na migogoro inayojitokeza mara kwa mara kati ya Wakulima na Wafugaji huku akiagiza wananchi watoe taarifa kwa kufuata ngazi husika ili watu waovu wanaohatarisha Amani katika Wilaya ya Mvomero wabainike na kuchukuliwa hatua mapema.

“Hakuna aliye juu ya sheria. Hatutamfumbia macho mtu yoyote anayehatarisha amani katika Wilaya yetu. Nawaomba wananchi watoe taarifa kuanzia ngazi ya Kijiji, Kata mpaka Wilaya ili tubaini watu waovu wanaohatarisha amani ili hatua stahiki za kisheria zichukuliwe.” Amesema Mkuu wa Wilaya. “Kama unamjua mfugaji anayehatarisha amani peleka jina lake katika ngazi ya Kijiji ili wafanye kazi na Polisi Kata ili haki itendeke ili mkulima alipwe stahiki yake  kwa kufuata miongozo ya kisheria. ” ameongeza Mkuu wa Wilaya.

Mkuu wa Wilaya pia amewaasa wafugaji wafuate njia za kisasa za kulisha mifugo ili kuepusha migogoro isiyokuwa na lazima kati ya Wakulima na Wafugaji. Ametoa maelekezo kuwa wafugaji wapewe mashamba ili waweze kupanda majani kwa ajili ya mifugo yao na kuepuka kulisha mifugo katika mashamba ya Wakulima. “Sitaki kuona wafugaji wanalisha mifugo yao katika mashamba ya wakulima. Tunao wafugaji wa kuigwa hapa Mvomero ambao wamepanda majani kwenye mashamba yao kwa ajili ya mifugo kama Maloroi, Shamba Kubwa. Huwezi kusikia hawa wanasababisha migogoro.Nitakuja kutoa mfano mwenyewe katika kupanda majani hapa.” Ameongeza Mkuu wa Wilaya.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ameiasa jamii ya Wanamvomero kukuemea vitendo vya kiovu vinavyoharibu maadili ya kitanzania. Amewaomba wananchi wafichue watu wote wanaoharibu watoto huku akiahidi kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watu wote watakaobainika kujihusisha na ulawiti wa watoto na kuharibu maadili ya Kitanzania kwa kutoa elimu isiyofaa kwa watoto. “Tayari kuna taasisi moja tumeibaini inafundisha watoto mambo yasiyofaa. Taasisi hii tayari tumeifungia.” Amesema Mkuu wa Wilaya.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.