• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MKUU WA WILAYA AENDELEA NA ZIARA KATA ZA LUBUNGO, MELELA, MSONGOZI NA MANGAE

Posted on: August 24th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amefanya ziara kutembelea wananchi na kutatua kero zao pamoja na kukagua miradi inayopata fedha katika Kata za Melela, Lubungo, Msongozi na Mangae ikiwa muendelezo wa utaratibu aliojiwekea kila wiki kutekeleza majukumu yake.

Katika ziara hiyo ambayo aliambatana na Kamati ya Usalama , wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Wakuu wa Taasisi za TAWA, TARURA, TANESCO pamoja na RUWASA, Mkuu wa Wilaya amepokea na kutatua kero mbalimbali za wananchi katika kata hizo.

Awali kabla ya kufanya Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kimambila tarehe 22 Agosti , Mkuu wa Wilaya alikagua shule ya Sekondari ya Lubungo iliyojengwa kwa fedha za UVIKO-19 na kujionea ukamilishwaji wa ujenzi wa madarasa ya shule hiyo huku akiagiza mamlaka husika zikamilishe usajili wa shule hiyo kwani wananfunzi wanatembea umbali mrefu sana umbali wa jumla wa kilomita 44 kwenda Shule ya Sekondari Mongola.

Akitoa maagizo hayo, Mkuu wa Wilaya ameitaka Ofisi ya Uthibiti Ubora Wilaya ya Mvomero kuipa kibali shule hiyo ili kuwaondolea wanafunzi hao adha ya umbali pamoja na hatari ya kujeruhiwa au kuuliwa na tembo kwani Kata hiyo ipo karibu sana na hifadhi ya Taifa ya Mikumi na ni njia ya tembo hivyo ni rahisi sana wanafunzi hao kukutana na wanyama hao pindi waendapo au watokapo shuleni.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ametaka kushughulikiwa kwa haraka kwa migogoro ya mipaka iliyopo katika ya Wilaya ya Mvomero na Manispaa na Morogoro huku akimuagiza Afisa Ardhi afanye haraka kuandaa mkutano kati ya viongozi wa pande hizi mbili ili watoe matamko swala la mgogoro huu limalizwe.

Mkuu wa Wilaya pia amewata Watumishi wa Serikali ambao hawaishi maeneo yao ya kazi kurudi haraka katika maeneo hayo kwani wananchi wanahitaji huduma za watumishi hao ziwe karibu muda wote.

Mkuu wa Wilaya pia baadae aliendelea na ziara katika Kata ya Melela ambapo alifanya mkutano wa hadhara na wananchi huku akitaka viongozi kushughulika ngazi ya Kijiji na kata kushughulikia kero za wananchi ambazo zipo ndani ya uwezo wao mapema kabla hazijafika ngazi za juu.

Katika mkutano huo wa hadhara pamoja na mambo mengine, amewataka wananchi kufuata utaratibu pindi wanapohitaji huduma fulani kutoka serikalini kama ununuzi wa ardhi kwa ajili ya shughuli mbalimbali au kuunganishiwa umeme kwani wasipofuata utaratibu uliowekwa na Serikali wanajiweka kwenye hatari ya kutapeliwa na kujiwekea wakati mgumu.

Katika kata za lubungo, Melela, Msongozi, Doma na Mangae Mkuu wa Wilaya aliongelea mambo mbalimbali ila dhima kuu ikiwa ni kero zinazosababishwa na wanyama waharibifu aina ya tembo kwani katika kata hizi zote nne, mashamba ya wakulima yamekuwa yakivamiwa na kuliwa hivyo kuwasababishia wananchi hasara kubwa kiuchumi. Pia vifo vingi vimeripotiwa katika maeneo hayo kwa kuwa yanapakana kwa karibu na Hifadhi ya Taifa Mikumi.

Masuala mengine ambayo Mkuu wa Wilaya aliyatatua katika kata hizo ni umeme, elimu, maji, migogoro ya wakulima na wafugaji pamoja na masuala mbalimbali za kijamii.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.