• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MIAKA 63 YA UHURU, WATANZANIA WAASWA KUWA NA MIOYO YA KUJITOLEA KULIENDELEZA TAIFA

Posted on: December 8th, 2024

Katika maadhimisho ya miaka 63 ya uhuru wa Tanganyika, Watanzania wameaswa kuwa na mioyo ya kujitolea pamoja na uzalendo na kushiriki kikamilifu katika juhudi za kulijenga na kuliendeleza taifa.

Akihutubia Desemba 8, 2024 katika kongamano la miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara sherehe za uhuru lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Ualimu Muhonda, Wilayani Mvomero, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Ndg. Saidi Nguya amewahimiza wananchi kuenzi uhuru walioupata kwa kujituma, kushirikiana, na kuchangia maendeleo ya nchi katika sekta zote.

"...utapewa unachopewa lakini lazima tutangulize moyo wa kujitolea ndiyo silaha ya maendeleo yetu..." amesisitiza Ndg. Nguya.

Akinukuu maneno ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyoyatoa mwaka 1988 wakati akizungumza na wazee wa Mkoa wa Tabora, Mwl. Nyerere alisisitiza kuwa "kama tunataka kupata maendeleo ya haraka ni lazima kama nchi tujenge mioyo ya kujitolea".

Aidha, Katibu Tawala huyo amewataka vijana, ambao ni zaidi ya nusu ya idadi ya watu nchini, kutumia fursa zilizopo kujenga taifa lao kwa moyo wa kujitolea, ubunifu, na uzalendo, huku akisisitiza kuwa roho ya kujitolea ni urithi unaopaswa kudumu kwa vizazi vyote.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Linno Mwageni ameipongeza na kuishukuru Serikali za awamu zote sita kwa juhudi zilizofanyika hadi sasa kwani nchi imepiga hatua mbalimbali za maendeleo kiuchumi, kijamii na kisiasa. Ameongeza kuwa bado mapambano yanaendelea ili kupata uhuru wa kifikra na uchumi ili kujenga taifa la kizalendo.

Naye Diwani wa Kata ya Muhonda Mhe. Rashid Juma ametumia kongamano hilo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini ambayo watanzania wanakila sababu ya kumpongeza kwa hilo.

Akitoa neno la shukrani kwa Viongozi na wageni waliohudhuria kongamano hilo mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho cha ualimu Muhonda amesema kupitia kongamano hilo wao kama wanafunzi hususan wa kikazi cha miaka ya 2000 wamejifunza mengi ikiwemo uzalendo.

Sherehe za uhuru mwaka huu 2024 zinatawaliwa na kaulimbiu inayosema "Uongozi Madhubuti na Ushirikishwaji wa Wananchi ni Msingi wa Maendeleo yetu"

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.