• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MFUMO WA STAKABADHI GHALANI MKOMBOZI KWA WAKULIMA WA KAKAO, WATAKIWA KUTOA TAARIFA KUUIMARISHA

Posted on: October 20th, 2024

Mfumo wa stakabadhi ghalani umetajwa  kuwa mkombozi kwa wakulima wa zao la kakao hapa nchini hususan wakulima wa Mhonda Wilayani Mvomero kwani  umeboresha maisha na kuimarisha uchumi wao kwa kuuza zao hilo kupitia mfumo huo kwa bei nzuri sokoni na kwamba umewasaidia kuepuka unyonyaji wa madalali na kupata thamani halisi ya mazao yao.

Hayo yamebainishwa Oktoba 20, 2024 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deo Mwanyika wakati wa akizungumza na wakulima wa zao hilo kwenye kitalu cha kakao kilichopo katika Kata ya Mhonda.

Mhe. Mwanyika amesema lengo la Serikali lilikuwa ni kuhakikisha kuwa mkulima wa kakao anapata bei nzuri ili aweze kuinuka kiuchumi. Akielezea mfumo huo amesema kuwa ni mfumo mzuri  ambao unamsaidia mkulima kupata bei halisi ya zao hilo huku akisema kuwa changamoto zilizoainishwa na wananchi zitafanyiwa kazi na kutoa wakulima kutoa taarifa kwa wakati ili kuuimarisha mfumo huo.

"...mimi nitoe wito ndugu zangu tutoe ushirikiano ili tuuimarishe huu mfumo, uimarike zaidi kama tunajua kuna watu ambao pengine wanakwepesha hawataki kuleta au wanafanya ujanja ujanja tutoe taarifa kwa muda kwa wakati kwa viongozi wetu..." amesema Mhe. Mwanyika.

Aidha, Mwenyekiti huo amesema wao kama Kamati ya Bunge wanatamani mfumo huo utumike na kwenye mazao mengine kutokana na manufaa yake kwa wakulima kwa sababu pale ambapo walipokuwa hawapati faida sasa wanapata faida.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe (Mb) amesema ziara hiyo imelenga kuangalia mfumo wa stakabadhi ghalani na jinsi unavyowanufaisha wakulima wa zao la kakao huku akimuhakikishia Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuwa changamoto zote zilizoainishwa na wakulima zinazohusiana na mfumo pamoja na mauzo Serikali itazifanyia kazi ili kuhakikisha kuwa mfumo unaimarika zaidi.

Amoeongeza kuwa Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kumkomboa mkulima kwa kuongeza tija ya uzalishaji kwenye eneo dogo huku akibainisha katika maeneo mengi hapa nchini mavuno yameongezeka kutokana na uwepo wa pembejeo za kilimo na kuongezeka kwa bajeti ya kilimo.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli akitoa neno la shukrani kwa kamati hiyo ya Bunge amesema maelekezo na ushauri uliotolewa na wajumbe wa kamati hiyo pamoja na changamoto zilizoelezwa na wakulima zitafanyiwa kazi kuhakikisha kuwa mkulima wa kakao Wilayani Mvomero anapata faida.

Nao wakulima wa zao la kakao waliofaidika na mfumo wa stakabadhi ghalani akiwemo Bw. Boniface Mahenge amesema awali kabla ya mfumowa stakabadhi ghalani walikuwa wanauza kwa bei ya hasara kuanzia shilingi 2000 lakini mfumo huo umesaidia bei kupanda hadi kufikia shilingi 17000 na zaidi. Pia amesema kupitia mfumo huo ameweza kuwaendeleza kimasomo watoto wake wawili na kujenga nyumba ya kisasa.

 MWISHO.  

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.