• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MAFUNZO KWA MAAFISA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NGAZI YA KATA YAHITIMISHWA, WASISITIZWA KUWA MAKINI UTUNZAJI WA VIFAA

Posted on: February 24th, 2025

Mafunzo kwa Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya kata katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero yamehitimishwa huku washiriki wakisisitizwa kuwa makini katika utunzaji wa vifaa vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

Mafunzo hayo yalilenga kuwawezesha maafisa hao kupata uelewa wa kina kuhusu taratibu za uandikishaji, matumizi sahihi ya vifaa kama vile mashine za BVR (Biometric Voter Registration) na umuhimu wa uhifadhi wa nyaraka muhimu za wapiga kura.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Afisa Muandikishaji Msaidizi Jimbo la Mvomero Bi. Mary Kayowa amesema kuwa vifaa hivyo vimenunuliwa kwa gharama kubwa hivyo Maafisa hao wametakiwa kuwa makini katika utunzaji wake ili kuepusha uharibifu ama upotevu ambao utaathiri zoezi la uandikishaji.

"...kwa hiyo kutokuwa makini katika utunzaji wa vifaa hivi utapelekea athari kubwa katika ukamilishaji wa zoezi hili..." amesema Bi. Mary

Sambambana hilo, Afisa Muandikishaji huyo amewataka kuzingatia muda wa kufungua na kufungwa kwa vituo vya kuandikisha wapiga kura, akisisitiza kuwa vituo vifunguliwe kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni.

Pamoja na hayo, Maafisa Waandikishaji wametakiwa kuhamasisha Wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la uboreshaji wa daftari ambapo zoezi hilo litaanza tarehe 01-07/3/2025

Nao, Maafisa Waandikishaji wasaidizi  wamewashukuru na kuwapongeza Maafisa kutoka Tume Huru ya Uchaguzi (iNEC) kwa mada nzuri huku wakiahidi kuwa zoezi hilo litakamilika kwa asilimia 100.

"Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora"

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.