• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

Posted on: March 19th, 2025

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Mvomero imekipongeza na kushukuru Kiwanda cha Sukari Mtibwa kwa juhudi zake za kusaidia wananchi kwa kurejesha mto Diwale kwenye mkondo wake wa asili, hatua inayolenga kuboresha mazingira na kuwaondolea adha ya mafuriko wakazi wa eneo hilo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Machi 19, 2025 Mwenyekiti wa Kamati ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Judith Nguli amesema juhudi za kiwanda hicho ni mfano mzuri wa ushirikiano kati ya sekta binafsi, Jamii na Serikali katika kutunza mazingira na kulinda vyanzo vya maji pamoja na kuokoa maisha ya watu.


"...ujio wetu huu tumekuja kwa ajili ya kutoa shukrani kwa kazi kubwa inayoendelea hapa kwenye mto Diwale ...Kampuni hii ya Mtibwa imebeba dhamana ya kutusaidia sisi Serikali tunasema asante..." Amesema Mkuu wa Wilaya.


Aidha, amesema kuwa wakazi wanaoshi karibu na mto huo wamekuwa wakiathirika na mafuriko kutokana na mto huo kuacha njia yake, hivyo kitendo cha Kampuni ya Mtibwa kurudisha mto kwenye mkondo wake ni msaada mkubwa kwa wakazi wa maeneo hayo.


Sambamba na hilo, Mhe. Nguli amesema kuwa Serikali imeandaa mpango mkakati wa muda mrefu wa kuboresha maeneo yote yenye changamoto ya mto kuhama kwenye mkondo wake ili kuhakikisha kuwa wananchi wanaendelea kuwa salama wakati wote hususan kipindi cha mvua.


Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya imetoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kushirikiana na serikali na jamii katika kutekeleza miradi kama hiyo ya kuwasaidia wananchi.


Kwa upande wake, mwakilishi wa Kiwanda cha Sukari Mtibwa Bw. Moses Tenda amesema kuwa mradi huo ni sehemu ya wajibu wao wa kusaidia jamii inayozunguka kiwanda hicho. Aidha, amesema mradi huo utaendela hadi mwezi Aprili mwaka huu, huku akibainisha kuwa Kampuni ya Mtibwa itaendelea kutoa msaada kwa wananchi pale ambapo inahitajika.


Pamoja na hayo, Bw. Moses ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira mazuri ambayo yamewavutia wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji mbalimbali hapa nchini kufanya shughuli

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.