• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

KAMATI ZA MIKOPO NGAZI YA KATA ZATAKIWA KUTENDA HAKI

Posted on: October 22nd, 2024

Kamati za huduma ya mikopo ya asilimia 10 ngazi ya kata wilayani Mvomero zimetakiwa kuhakikisha zinatenda haki katika mchakato wa kupendekeza vikundi vyenye sifa ya kupata mikopo hiyo.

Agizo hilo limetolewa Oktoba 22, 2024, na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Judith Nguli, wakati akifungua mafunzo kwa kamati za huduma ya mikopo ngazi ya kata kwa tarafa za Mgeta na Mlali, yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Mzumbe.

Mhe. Nguli amesisitiza umuhimu wa kamati hizo kufuata taratibu na miongozo iliyowekwa ili kuhakikisha mikopo inawanufaisha wananchi wote bila upendeleo. Amesema mikopo hiyo inapaswa kuelekezwa kwa vikundi vyenye sifa na uwezo wa kurejesha mikopo ili kufikia malengo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha maisha ya wananchi na kukuza uchumi wa Wilaya.

Aidha, amewataka wajumbe wa kamati kuwa waadilifu na kutanguliza maslahi ya umma, huku akionya dhidi ya vitendo vya rushwa na upendeleo vinavyoweza kuathiri mchakato wa utoaji mikopo.

Naye, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Mashaka Malole amesema Halmashauri hiyo imetenga zaidi ya shilingi milioni 694 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya Vijana, Wanawake na wenye ulemavu vyenye sifa ya kupata  mikopo hiyo. Aidha, amebainisha baadhi ya sifa za kupata mikopo hiyo zikiwemo kuunda vikundi kuanzia watu watano, umri wa miaka 18 hadi 45 kwa vikundi vya vijana pia vikundi hivyo vinatakiwa viwevimesajiliwa.

Kwa upande wake Bi. Angel Charles akiwakilisha kundi la watu wenye ulemavu ameishukuru Serikali ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fursa kwa kundi hilo kupata mikopo ya 10 inayotolewa na Halmashauri huku akitoa wito kwa kundi hilo kujitokeza kuchukua mikopo hiyo ambayo itasaidia kuinua hali zao za kiuchumi.

Akizungumza wakati akihitimisha mafunzo hayo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bi. Sia Ngao amewashukuru Watendaji wa Kata waliohudhuria mafunzo hayo na kuwataka kushirikiana na maafisa maendeleo ya jamii wa Kata ili kupata vikundi vyenye tija.

Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati za mikopo katika kutekeleza majukumu yao kwa uwazi, haki, na uwajibikaji, ili kufikia malengo ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.