• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

JESHI LA AKIBA LATAKIWA KUZUIA NA KUDHIBITI MADAWA YA KULEVYA

Posted on: December 21st, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewataka Askari wa Jeshi la Akiba kushirikiana kwa karibu na vyombo vingine vya usalama katika vita dhidi ya madawa ya kulevya ambayo ni tishio kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya Taifa.

Mhe. Nguli ametoa kauli hiyo Novemba 21, 2024 wakati akifunga mafunzo ya Jeshi la Akiba kundi la 9 mwaka 2024 ambapo kwa mwaka huu yamefanyika katika Tarafa ya Mlali.

Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza umuhimu wa jeshi hilo kuchukua hatua madhubuti za kuzuia biashara haramu ya madawa ya kulevya ikiwemo bangi na kuwafikisha wahusika mbele ya sheria ili kuwa na Taifa lenye ustawi.

Aidha, amesema kuwa madawa ya kulevya siyo tu yanaharibu maisha ya vijana, bali pia yanachangia ongezeko la uhalifu na kudhoofisha uchumi wa nchi.

"...kikubwa mkazuie madawa ya kulevya...madawa ya kulevya yanaharibu Taifa, yanaharibu wananchi kiakili ..." amesema Mkuu wa Wilaya.

Sambamba na hilo Mhe. Nguli amewataka Askari hao kutojihusisha na vitendo vya uharifu bali watumie mafunzo waliyopata kuzuia uharifu na kulinda amani.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya amewataka wagombea wa vyama vya Siasa ambao wanafanya kampeni zao kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa  unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2024 kuhakikisha kuwa wanafanya kampeni hizo bila kuvunja sheria zilizowekwa na kwamba Serikali itamchukulia hatua za kisheria kwa atakaye kiuka.

Kwa upande wake Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Mvomero amesema mafunzo hayo hufanyika kila mwaka ambapo kwa mwaka huu 2024 yamefanyika katika Tarafa ya Mlali huku yakitarajiwa kufanyika Tarafa ya Turiani mwaka ujao. Aidha, ameongeza kuwa wahitimu wa mwaka huu wapo 149 kati yao wanaume ni 96 na wanawake 50 huku wengine 13 wakishindwa kuendelea kutokana na sababu mbalimbali.

Kwa upande wao wahitimu wa mafunzo hayo kupitia Risala iliyosomwa mbele ya Mkuu wa Wilaya wamesema mafunzo hayo yalianza Julai Mosi, 2024 yakiwa na wanafunzi 159 lakini waliofanikiwa kuhitimu ni 146. Aidha, wamewasilisha ombi kwa Serikali wakiomba kupatiwa mikopo ili waweze kujishughulisha na ujasiriamali.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.