• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

HAKI IKATAWALE BILA UPENDELEO KWENYE MIKOPO YA VIKUNDI - DC NGULI

Posted on: October 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli ametoa wito kwa Kamati za huduma ya mikopo ngazi ya Kata za Tarafa ya Turiani na Mvomero kuhakikisha kuwa haki inatawala bila upendeleo wakati wa mchakato wa kupata vikundi vyenye sifa ya kupata mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri.

Akizungumza Oktoba 23, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa kamati hizo yaliyolenga kuwajengea uelewa juu ya masuala ya mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu, Mhe. Nguli amesema kuwa ni muhimu kila kundi lipate fursa sawa ya kupata mikopo ili kuwezesha maendeleo endelevu.

Mkuu huyo wa Wilaya ameongeza kuwa utoaji wa mikopo kwa wananchi ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi 2020 - 2025 ya Chama cha Mapinduzi - CCM Ibara ya 23 na 24 ambapo CCM iliahidi kupambana na umaskini pamoja na kuwawezeshawananchi kiuchumi.

"Kikubwa Haki ikatawale bila upendeleo" amesema Mhe. Nguli

Aidha, Mhe. Nguli amewasisitiza Wajumbe wa kamati hizo kutoa elimu na ushauri kwa vikundi ili vianzishe miradi inayozalisha na yenye tija kwani kwa kufanya hivyo itawasaidia wanakikundi kumudu marejesho ya mikopo waliyoiomba.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri Bi. Sia Ngao amesema kwa mujibu wa muongozo mpya wa utoaji wa Mikopo ya asilimia 10 umezielekeza Halmashauri kuwa na Kamati za mikopo ngazi ya Kata  kwa kuwa ngazi hiyo ndiko vikundi vingi vinapatikana huku akibainisha lengo la kuundwa kwa Kamati hizo ni kuwasaidia maafisa maendeleo ya jamii katika usimamizi wa mikopo.

Kamati hizo za Mikopo ngazi ya Kata zinaundwa na Watendaji wa Kata, Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Kata, Watendaji wa Vijiji, Maafisa Ugani, Waratibu wa elimu ngazi ya Kata na Askari Kata.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.