• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DIVISHENI YA HUDUMA ZA AFYA MVOMERO YAPONGEZWA KUVUKA LENGO UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS

Posted on: July 9th, 2025

Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero imepongezwa kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa Serikali wa GoT-HoMIS, hatua inayodhihirisha ufanisi wa usimamizi na uwajibikaji katika utoaji wa huduma za afya.

Pongezi hizo zimetolewa Julai 9, 2025 na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw. Paulo Faty wakati wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa utoaji huduma za Afya kwa mwaka 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Mkurugenzi huyo amsema mafanikio hayo yanatokana na ushirikiano mzuri baina ya viongozi wa vituo vya kutolea huduma za afya na watendaji wa idara ya afya ngazi ya wilaya huku akiwapongeza kwa kuvuka lengo kwa asilimia 127.


Kwa mujibu wa takwimu zilizowasilishwa, hadi kufikia mwisho wa mwezi Juni 2025, Idara ya Afya ilikuwa imekusanya zaidi ya asilimia 127 ya lengo la mapato ya ndani yaliyopangwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kupitia mfumo wa GoT-HoMIS.


Sambamba na pongezi hizo Bw. Paulo Faty amewataka kuendelea kutoa huduma bora za Afya huku akiwasihi kuwa na lugha za staha pindi wanapowahudumia wateja wao kwani kumekwa na malalamiko kwa baadhi ya watoa huduma za Afya wamekuwa wakitoa lugha zisizo za staha na kwamba Serikali haitasita kuwachukulia hatua.


Naye Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Dkt. Phillipina Phillipo amesema mfumo wa GoT-HoMIS umeboresha uwazi, ufuatiliaji na udhibiti wa mapato, na hivyo kusaidia kuboresha huduma za afya kwa wananchi.


Aidha, amebainisha kuwa idara ilijiwekea malengo ya kukusanya shilingi milioni 479,000,000 kupitia mfumo huo ambapo hadi kufikia Juni 29, 2025 wamefanikiwa kukusanya shilingi milioni 607,463,534 ambayo ni sawa na asilimia 127.


Kwa upande wao, baadhi ya waganga wafawidhi kutoka vituo vya afya na zahanati walieleza kuwa mafanikio hayo pia yametokana na mafunzo ya mara kwa mara kuhusu matumizi ya mfumo huo pamoja na ufuatiliaji wa karibu kutoka kwa viongozi wa afya ngazi ya wilaya.


MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.