• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DED MVOMERO AWATAKA WAUGUZI, MATABIBU KUTUMIA LUGHA NZURI KWA WAGONJWA

Posted on: February 13th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Linno P. Mwageni amewataka wauguzi na matabibu kutumia lugha nzuri kwa wagonjwa ili kuwasogeza karibu na huduma za hospitali kwani kutoa huduma mbaya na kutowasikiliza wagonjwa ni chanzo cha kuwaweka mbali na huduma hizo na kuwafanya wakimbilie kwa waganga wa kienyeji.

Mwl. Mwageni ameyasema hayo mapema Februari 13, 2024 wakati akizungumza na maafisa Afya, matabibu na wauguzi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya vilivyopo ukanda wa Mlali, Mgeta na Melela akiwa na lengo la kuwakumbusha wajibu wao katika zoezi la chanjo ya surua na rubella kwa watoto wenye umri wa miezi 9 na chini ya miaka mitano litakalofanyika kuanzia tarehe 15.02.2024 mpaka tarehe 18.02.2024 katika Vituo 75 vya kutolea huduma za Afya vilivyopo katika Wilaya hiyo.

Kampeni hiyo ina lengo la kuchanja watoto wapatao 52,000 katika Wilaya ya Mvomero. Aliwataka waganga wa Vituo vya kutolea huduma za Afya kutangaza huduma hiyo kwa njia ya vipaza sauti katika maeneo mbalimbali yenye mkusanyiko. Mkurugenzi huyo ameahidi kutoa zawadi kwa Kituo cha kutolea huduma ya Afya kitakachofanya vizuri katika uchanjaji na kuvuka lengo la asilimia 100.

Aidha, Mwl. Linno alivitaka Vituo vinavyopokea fedha za miradi kutoka Serikali Kuu, Wafadhili na Makusanyo ya fedha za papo kwa papo na CHF kuwa makini katika matumizi ya fedha hizo na kuagiza zitumike kadri maelekezo yanavyotaka.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mtendaji huyo amevipongeza Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa kukusanya vizuri mapato kwa kutumia Mfumo wa GoTHOMIS. Pia ameelekeza Vituo hivyo kutumia Mfumo wa NEST katika kufanya taratibu za Manunuzi katika Ngazi ya Makao Makuu na Vituoni.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kikao hicho Ndg. Jackson Nyaonge alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kwa kutoa maelekezo na kuahidi kusimamia chanjo na kuvuka lengo la asilimia 100.

Baada ya kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji alikagua mradi wa vyoo, shimo la kutupia kondo la nyuma, miradi hii imejengwa kwa fedha za EP4R kiasi cha Sh. 54,000,000 na jengo la kuhifadhia maiti.

MWISHO

 

 

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.