• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DED MVOMERO ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA SRWSS KATIKA VITUO VYA AFYA

Posted on: January 17th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Mwl. Linno Mwageni ameonyesha kuridhishwa na hatua kubwa zilizofikiwa katika utekelezaji wa Mradi wa Usambazaji Endelevu wa Maji Vijijini na Usafi wa Mazingira (SRWSS) katika vituo vya kutolea huduma za afya wilayani humo.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo, iliyofanyika Januari 16 na 17, 202, Mwl. Linno amesema kuwa mradi huo ni suluhisho muhimu kwa changamoto ya upatikanaji wa maji safi na mazingira bora katika vituo vya afya, ambavyo ni sehemu muhimu ya kuboresha huduma kwa wananchi wa Mvomero.

Aidha, Mkurugenzi huyo amesisitiza kuwa Halmashauri itaendelea kusimamia kikamilifu miradi kama hii ili kuhakikisha inawanufaisha wananchi kwa muda mrefu. Pia ametoa wito kwa wasimaizi wa vituo hivyo kuhakikisha wanapanda miche ya mazao ya kimkakati kama vile karafuu, Kokoa na Chikichi kuzunguka eneo la kituo.

Mradi wa SRWSS unalenga kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama vijijini ukiambatana sambamba na ujenzi wa vyoo bora pamoja na matumizi sahihi ya vifaa vya kunawia mikono kwa maji tiririka katika ngazi ya kaya na taasisi zote zilizopo katika vijiji 45 vya wilaya ya Mvomero.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Dkt. Philipina Philipo amesema Halmashauri imepokea jumla ya kiasi cha shilingi 490,118,231.39 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya usafi katika vituo 7 vya kutolea huduma za Afya kwa awamu mbili.

Awamu ya kwanza Halmashauri ilipokea kiasi cha Tsh. 238,848,519.12 na Tshs. 160,666,666 sawa na asilimia 67.26% ya fedha zilizotumika katika ujenzi wa miundombinu ya usafi wa mazingira katika Zahanati ya Madizini, Lusanga na Kituo cha Afya Mlali na Tshs. 78,181,853.12 sawa na asilimia 32.73% ya fedha zilitumika katika usimamizi na ufuatiliaji wa ujenzi wa miradi pamoja na uhamasishaji wa ujenzi wa vyoo bora na matumizi ya vibuyu chirizi katika ngazi ya kaya.

Aidha, ameongeza kuwa kwa awamu ya pili Halmashauri ilipokea kiasi cha Tsh. 251,269,712.27 ambapo Tsh. 200,000,000 sawa na 79.59 % zimeelekezwa katika ujenzi wa miundombinu ya usafi katika vituo 4 vya kutolea huduma za Afya ambavyo ni Kituo cha Afya Mvomero, Kituo cha Afya Mgeta, Zahanati ya Kidudwe na Zahanati ya Mikongeni. Kiasi cha Tshs. 51,269,712.27 sawa na 20.40 % zimetumika katika shughuli za usimamizi wa mradi, uratibu wa zoezi la uhamasihaji wa ujenzi wa vyoo bora na matumizi ya vibuyu chirizi.

Halmashauri imefanikiwa kuvuna fedha kiasi cha Tsh. 633,319,750 baada ya kutekeleza mradi huu kwa ufanisi mkubwa. Fedha hii itaendelea kuboresha miundombinu ya usafi wa mazingira kwenye vituo vingine vya kutolea huduma za afya.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.