• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DED MVOMERO AAGIZA MAAFISA KILIMO KATA, VIJIJI KUANZISHA MASHAMBA DARASA SHULLE ZA MSINGI, SEKONDARI

Posted on: November 19th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Mwl.Linno Mwageni amewaagiza maafisa kilimo ngazi ya Kata na Vijiji katika Halmashauri hiyo kuhakikisha wanaratibu na kuanzisha mashamba darasa ya mazao yanaolimwa zaidi kwenye eneo husika katika kila shule ya msingi na sekondari ndani ya wilaya hiyo.

Akizungumza Novemba 19, 2024 wakati wa kikao kazi cha wadau wa kilimo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, Mwl. Linno amesema hatua hiyo inalenga kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kilimo cha kisasa tangu wakiwa wadogo, ili kuwaandaa kwa maisha ya kujitegemea na kuongeza uzalishaji wa mazao kwa tija.


"...jamani shule zote za msingi na sekondari lazima ziwe sehemu ambazo kunakuwa na mashamba darasa..." amesema Mwl. Linno

Ameongeza kuwa mashamba darasa hayo pia yatawezesha jamii zinazozunguka shule kujifunza mbinu bora za kilimo kupitia mafunzo yatakayokuwa yakitolewa na walimu kwa kushirikiana na maafisa kilimo.

Aidha, amelipongeza shilika la SUGECO (Ushirika wa wajasiriamali wahitimu wa chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine) kwa kuja na mradi ambao utawainua vijana kiuchumi kupitia kilimo huku aliahidi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha kuwa Vijana wa Halmashauri hiyo wanajikita kwenye kilimo.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa YEFFA (Youth Entrepreneurship for future of food and agriculture) Bi. Jacqueline Jonathan kutoka shirika la SUGECO amesema kuwa mradi huo una lengo la kuimarisha ushirikishwaji na uwezeshwaji wa vijana katika kuzalisha ajira kupitia sekta ya kilimo biashara.

Mradi umefadhiliwa na Mastercard Foundation na utadumu kwa kipindi cha miezi 36(miaka 3) ambapo umeanza rasmi Sept 2024 - Aug 2027.

Bi. Jacqueline ameongeza kuwa mazao yaliyochaguliwa katika mradi huu ni Alizeti, Mahindi, Maharahe, Soya, Mpunga na mazao ya bustani. Hata hivyo, amesema matarajio ya mradi huu ni kupata kanzi data yenye taarifa kamili za vijana wanaojishughulisha kwenye mnyororo wa thamani wa kilimo na sekta nyingine ili kuboresha ushirikishwaji na uwezeshwaji kupitia program mbalimbali za maendeleo katika sekta ya kilimo hapa nchini, mradi huu pia utawanufaisha vijana 17500 wa Wilaya ya Mvomero.

Mpango huu unakuja wakati ambapo serikali inaendelea kuhamasisha matumizi ya kilimo cha kisasa ili kufanikisha lengo la kujitosheleza kwa chakula na kuongeza pato la taifa.

MWISHO.


Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.