• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DED LINNO AWASISITIZA MAFUNDI, WAZABUNI MVOMERO KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA NeST

Posted on: November 18th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Mwl. Linno Mwageni amewataka mafundi na wazabuni wote ndani ya halmashauri hiyo kuhakikisha wanajisajili kwenye Mfumo mpya wa Ununuzi Umma NeST ili kushiriki kwenye fursa mbalimbali za miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Mwl. Linno ameyasema hayo Novemba 18, 2024 wakati akifungua mafunzo ya siku moja ya mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma - NeST kwa Mafundi na Wazabuni wa Halmashauri hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri.

Akizungumza katika mafunzo hayo Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema mfumo wa NeST ni nyenzo muhimu iliyowekwa na serikali ili kuimarisha uwazi, ufanisi, na uadilifu katika manunuzi ya Umma.

"...Mafundi na wasambazaji wa bidhaa tujisajili kwenye mfumo ili pesa zinazoingia ndani ya Wilaya yetu basi tuzifanyie kazi..." amesisitiza Mwl. Linno.

Aidha, ameongeza kuwa usajili kwenye mfumo huo ni sharti la kisheria kwa watoa huduma wote wanaotaka kushiriki katika zabuni za serikali huku akibainisha kuwa kutokujisajili kutawazuia mafundi na wazabuni kupata nafasi ya kushiriki kwenye miradi mikubwa inayofadhiliwa na serikali katika Wilaya hiyo.

Sambamba na hilo, Mwl. Linno amesema Halmashauri itafanya mpango ea kuhakikisha kuwa mafundi wote wa Wilaya hiyo wanapatiwa vyeti vya taaluma ya ufundi ili waweze kutambulika zaidi lakini pia vyeti hivyo vitawasaidia kujisajili kwenye mfumo huo wa NeST.

Kwa upande wake, Afisa Manunuzi wa Halmashauri hiyo Bi. Aimana Nkya amewahakikishia watoa huduma kuwa mfumo wa NeST utarahisisha mchakato wa malipo na zabuni, huku ukipunguza changamoto za urasimu zilizokuwepo awali. Hata hivyo, amewataka kutekeleza miradi kwa ubora unaotakiwa na kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati.

Naye, Mhandisi wa ujenzi wa Halmashauri Bw. Michael Mangoli amewataka wasambazaji wa bidhaa kuhakikisha kuwa wanafikisha vitendea kazi kwa wakati ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Nao, mafundi waliohudhuria mafunzo hayo wameishukuru Halmashauri kwa mafunzo hayo ambayo yatawasaidia kupata fursa za kutekeleza miradi ya Serikali. Aidha, wameomba mchakato wa vyeti ufanyike haraka ili waweze kutambulika rasmi.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.