• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DED LINNO AKABIDHI PIKIPIKI IDARA YA AFYA KUSAIDIA USIMAMIZI WA CHANJO, MIRADI YA USAFI KATIKA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

Posted on: January 16th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mwl. Linno Mwageni amekabidhi pikipiki mpya nne kwa Idara ya Afya kwa lengo la kuboresha usimamizi na ufuatiliaji wa huduma za chanjo pamoja na ufuatiliaji wa miradi ya usafi na mazingira katika vituo vya kutolea huduma za Afya katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki hizo iliyofanyika Januari 16, 2025 katika ofisi za Halmashauri, Mwl. Linno amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi kwa haraka na ufanisi zaidi.

"...Pikipiki hii unaweza ukakiona ni chombo kidogo sana lakini ikifanya kazi zilizotarajiwa, hii italeta matokeo makubwa sana hasa katika sekta ya chanjo na masuala ya usafi..." amesema Mwl. Linno.

Aidha, amemtaka Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa anawasimamia watumishi waliopokea usafiri huo ili watumie vyombo hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa na kwamba atakaye kiuka atachukuliwa hatua ikiwemo kunyang'anywa.

Naye, Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt. Philipina Philipo amesema pikipiki mbili zitatumika katika usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya usafi wa mazingira katika Kata za Mlali na Dakawa, pikipiki nyingine  mbili zitatumia katika masuala ya chanjo ambapo moja itatumika kwa ngazi ya CHMT (Timu ya usimamizi na ufuatiliaji wa huduma za Afya ngazi ya Halmashauri) na nyingine kituo cha Afya Mgeta.

Kwa upande wao baadhi ya watumishi waliokabidhiwa pikipiki hizo akiwemo Afisa Afya wa Kata ya Dakawa Bi. Irene Mtenji amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji, Mganga Mkuu wa Wilaya kwa kuhakikisha kuwa watumishi hao wanapata usafiri. Aidha, amesema usafiri huo utasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku kutokana na kuwa baadhi ya maeneo kutofikika kwa urahisi.

Naye, Afisa Afya Bw. Benson Peter amesema pikipiki hizo zitasaidia katika kusimamia na kuratibu shughuli za afua za chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.