• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC NGULI AZINDUA BARAZA LA BIASHARA, ABAINISHA FURSA ZILIZOPO MVOMERO

Posted on: May 30th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amezindua rasmi Baraza la Biashara la Wilaya likiwa na lengo la kuimarisha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa maendeleo ya jamii na kiuchumi.

Akizungumza Mei 30, 2024 wakati akizindua baraza hilo kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo amesema Baraza hilo linajumuisha sekta za Umma na binafsi kujadili kwa pamoja masuala ya kimkakati katika kuboresha maslahi ya wafanyabiashara Wilayani humo.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amebainisha fursa mbalimbali ambapo wamewataka wafanyabiashara kujitokeza kuwekeza katika Wilaya hiyo, miongoni mwa fursa hizo ni pamoja na kilimo cha mazao ya biashara yakiwemo mazao ya kakao, karafuu, mpunga, fursa za ufugaji na viwanda.

“...unaruhusiwa kuja Halmashauri ukauliza utaratibu, ukapewa muongozo wa namna sahihi ya kutumia hizo fursa za Halmashauri yako...” amesema Mkuu wa Wilaya.

Katika hatua nyingine, Mhe. Nguli ametoa rai kwa wafanyabiashara kuacha tabia ya kuchepusha mapato huku akibainisha kuwa kitendo hicho kinapunguza mapato ya Halmashauri.

Naye Afisa Biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Nsubisi Kapula ameeleza vipaumbele vya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2024/2025 upande wa biashara ikiwemo ujenzi wa kituo cha mabasi Mlali, kuboresha kituo cha mabasi Manyinga, ujenzi wa masoko maeneo ya Mlali, Madizini na Dakawa, uwezeshaji wa miche ya kokoa, karafuu, Michikichi na Parachichi kwa wananchi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara (TCCIA) Wilaya ya Mvomero Bw. Juma Sangai amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kudhibiti matukio ya kiharifu hususan wizi katika maeneo ya Madizini ambapo kwa sasa wafanyabiashara wanaendelea na biashara zao hata nyakati za usiku.

Baraza la Biashara la Wilaya linaundwa na Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye Mwenyekiti, Wajumbe 40 kutoka Sekta za Umma na Binafsi, Wajumbe 10 wa Kamati tendaji pamoja na Kamati kazi ya baraza hilo la Wilaya.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.