• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC NGULI AWAONYA WATUMISHI JUU YA MATUMIZI MABAYA YA MALI YA UMMA

Posted on: September 18th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli amewaonya watumishi Wilayani humo juu ya matumizi mabaya ya mali za umma katika maeneo yao ya kazi kwani kwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria, taratibu na miongozo ya Utumishi wa Umma.

Mhe. Nguli ametoa onyo hilo Septemba 18, 2024 wakati akifungua mafunzo ya mfumo wa ukusanyaji taarifa na mapato kielektroniki yaani GoTHoMIS katika vituo vya afya na Zahanati zilizopo katika Wilaya hiyo, mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano huo Mkuu huyo wa Wilaya amewataka kuacha kutumia mali ya Umma kwa maslahi yao binafsi badala yake watumie mali hizo kama ilivyoelekezwa na Serikali na kwamba atakae bainika kukiuka atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma ikiwemo kufukuzwa kazi, kushushwa cheo au kupunguzwa mshahara.

"...kitu kinachoitwa mali ya umma usikichezee..." amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Nguli ametoa kauli hiyo baada ya kukamatwa kwa dereva wa gari la kubeba wagonjwa (Ambulance) la Kituo cha Afya Chazi kilichopo Wilayani humo kwa kosa la kubeba abiria kinyume na miongozo ya Wizara ya Afya huku akibainisha kuwa tayari dereva huyo amechukuliwa hatua za kisheria.

Akizungumzia mfumo huo wa GoTHoMIS, Mkuu huyo wa Wilaya amesema mfumo utasaidia kuongeza ukusanyaji wa mapato, upatikanaji wa takwimu za wagonjwa ambazo zitasaidia katika mipango ya uboreshaji wa Sekta ya Afya. Aidha, amewataka kwenda kufanyia kazi mfumo huo ili kuleta matokeo chanya katika Wilaya hiyo.

Awali wakati akimkaribisha Mkuu wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Dkt. Philipina Philipo amesema mfumo huo unarahisisha ufuatiliaji wa utoaji huduma za Afya, kujua idadi ya wagonjwa waliopata huduma na kiasi cha mapato yaliyokusanywa katika Zahanati au Kituo cha Afya husika.

Ameongeza kuwa mfumo wa GoTHoMIS uliokuwa ukitumika awali ulikuwa na mapungufu ikiwemo kupelekea kupotea kwa mapato ambao katika Wilaya hiyo Vituo 13 vilifungwa mfumo huo lakini kwa sasa ni Vituo vya Afya vyote na Zahanati vitafungwa mfumo huo mpya ambao ni rahisi kutumia.

MWISHO.                                

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.