• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC MVOMERO ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA SHULE MPYA YA KATA YA MKINDO

Posted on: August 15th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Maulid Dotto, ameonesha kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya kata ya Mkindo, akisema kuwa hatua hiyo itaondoa changamoto ya umbali pamoja na msongamano wa wanafunzi katika shule jirani na kuongeza fursa za kielimu kwa vijana wa eneo hilo.

Akizungumza alipotembelea mradi huo Agosti 15, 2025, Mkuu huyo wa Wilaya amesema ujenzi wa shule hiyo unakwenda sambamba na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha miundombinu ya elimu nchini.

“...kwenye ziara yangu miongoni mwa miradi iliyonifurahisha sana moja wapo ni huu katika kijiji cha Mkindo, mmefanya kazi nzuri sana..." amesema Mhe. Dotto.


Aidha, amewashukuru viongozi wa kijiji na kata kuhakikisha wananchi wanaendelea kushiriki kikamilifu kwenye ujenzi kwa kuchangia nguvu kazi na kufanikisha ukamilishaji wa majengo kwa muda uliopangwa huku akisisitiza kuwa waendelee na ukamilishaji ili shule hiyo ianze kupokea wanafunzi.


Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo amesema fedha za utekelezaji wa mradi huo ni zimetoka Serikali kuu ambapo zaidi ya shilingi milioni 528 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo. Ameongeza kuwa ujenzi huo unajumuisha vyumba nane vya madarasa, Jengo la utawala, Jengo la Tehama, Maabara mbili, maktaba pamoja na matundu ya vyoo, hata hivyo ujenzi umefikia asilimia 90 na matarajio ni kuwa hadi kufikia tarehe 30 Agosti 2025 itakuwa imekamilika kwa asilimia 100.


Nao baadhi ya wananchi wa Mkindo wamemshukuru Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa katika sekta ya elimu, wakieleza kuwa shule hiyo itapunguza gharama na umbali wa wanafunzi kutembea kufuata elimu katika kata nyingine.


Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • DC MVOMERO ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA SHULE MPYA YA KATA YA MKINDO

    August 15, 2025
  • DC MVOMERO AKAGUA MIRADI YA BARABARA TARAFA YA MGETA

    August 14, 2025
  • DC MAULID DOTTO AANZA ZIARA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    August 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.