• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC MVOMERO AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUFIKISHA HUDUMA ZA KIBINGWA MVOMERO

Posted on: June 4th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka huduma ya madaktari bingwa kwenye maeneo ya wananchi huku akibainisha kuwa kitendo hicho kinawapa watendaji wa Serikali ujasiri wa kuyasema mazuri yanayofanywa na Serikali ya Dkt. Samia.

Mhe. Nguli ametoa shukrani hizo Juni 4, 2024 wakati akizindua Kliniki Tembezi ya Madaktari bingwa wa Rais Samia Wilayani Mvomero ambapo Madaktari hao wameweka kambi ya siku tano katika Hospitali ya Wilaya ya Mvomero wanatarajia kutoa matibabu ya kibingwa kwa wananchi wa Wilaya hiyo.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema wananchi wanachangamoto mbalimbali za kiafya hususan za kibingwa, hivyo Serikali ya Dkt. Samia imeamua kuchukua hatua ya kuwasogezea huduma hizo kwenye maeneo yao.

“…niendeleee kumshukuru Mhe.  Rais Daktari Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo anatuvesha nguo sisi wasaidizi wake kwa sababu tumekuwa tukipita sehemu mbalimbali tunakuta changamoto za wananchi ni kubwa upande wa kiafya…”amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Nguli ametumia nafasi hiyo kuwa asa wananchi kuwapuuza watu wasiona mapenzi mema na Serikali ya Dkt. Suluhu Hassan kwamba haifanyikazi huku akibainisha kuwa Serikali hiyo inaendelea na juhudi za kuboresha Sekta ya Afya.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wananchi kujikinga dhidi ya magonjwa ya tumbo, kuhara na kutapika kwa kutumia maji safi na salama kabla au baada ya kula, baada ya kutoka chooni, kuosha matunda na mbogamboga pamoja na kula chakula cha moto.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Dkt. Philipina Philipo amebainisha kuwa mwananchi wamekuwa na mwitikio chanya ambapo siku ya kwanza ya huduma za kibingwa wameandikisha wagonjwa 114, hivyo ameendelea kuwahimiza  wananchi kujitokeza katika hospitali ya Wilaya ili wapate huduma hizo.

Dkt. Philipina ameeleza huduma zitakazotolewa na madaktari bingwa ikiwa ni pamoja na huduma ya magonjwa ya wanawake, huduma ya magonjwa ya ndani, huduma za watoto na watoto wachanga, upasuaji na huduma za ganzi na usingizi.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake ambaye pia ni kiongozi wa msafara huo amesema watakuwepo Hospitalini hapo kwa muda wa wiki moja lengo ni kutoa huduma za kibingwa ili kuwapunguzia gharama ya kufuata huduma hizo katika hospitali kubwa kama Muhimbili, KCMC, Benjamin Mkapa, Morogoro na maeneo mengine na huduma hizo zitatolewa katika Hospitali za Wilaya 185 hapa nchini.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WITO UMETOLEWA KWA WADAU, SERIKALI KUONGEZA JUHUDI KATIKA UTOAJI ELIMU YA HEDHI SALAMA VIJIJINI

    May 28, 2025
  • WAHE. MADIWANI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MLIMBA WATEMBELEA MVOMERO KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI UNAVYOWAKOMBOA WAKULIMA WA KAKAO

    May 24, 2025
  • MVOMERO KUUZA UFUTA KUPITIA STAKABADHI GHALANI KUANZIA MEI 20, 2025

    May 16, 2025
  • MKURUGENZI INEC AWASISITIZA WAANDHISHI WASAIDIZI, WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NGAZI YA KITUO KUZINGATIA MUDA WA KUFUNGUA VITUO VYA KUANDIKISHA WAPIGA KURA

    May 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.