• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC MVOMERO AHAMASISHA BODA BODA, MAMA LISHE KUJIANDIKISHA DAFTARI LA MKAAZI

Posted on: October 19th, 2024

DC Mvomero ahamasisha Boda boda, Mama lishe kujiandikisha Daftari la Mkaazi.

Ikiwa zoezi la kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga wa Serikali za Mitaa likielekea ukingoni, Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli ameendelea na juhudi za kuhamasisha makundi mbalimbali ya wananchi Wilayani humo yakiwemo waendesha boda boda, maguta na mama lishe kujiandikisha katika daftari hilo ili kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Mhe. Nguli ametoa rai hiyo kwa makundi hayo Oktoba 19, 2024 kwenye mkutano wa kuhamasisha wananchi kujiandikisha uliofanyika katika Kitongoji cha Mji Mwema huku akisisitiza umuhimu wa kujiandikisha mapema ili kuhakikisha wanatumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura na kuchagua viongozi wanaostahili.

Mkuu huyo wa Wilaya ameeleza kuwa kujiandikisha kwenye Daftari la wapiga Kura wa Serikali za Mitaa ni hatua muhimu kwa waendesha boda boda, kwani inawapa nafasi ya kushiriki kwenye maamuzi ya kitaifa yanayoweza kuleta mabadiliko katika sekta ya usafiri na huduma za jamii. Amesema kuwa ushiriki wao ni muhimu katika kuchagua viongozi watakaosaidia kuboresha mazingira yao ya kazi na kuleta maendeleo.

Kwa upande wa mama lishe, Mhe. Judith Nguli amewahimiza kujitokeza na kujiandikisha ili kuwa sehemu ya mchakato wa uchaguzi na kuhakikisha sauti zao zinasikika. Pia amebainisha kuwa kuchagua viongozi bora kunaweza kuleta fursa zaidi za kiuchumi kwa wanawake wajasiriamali, ikiwa ni pamoja na mikopo na mafunzo ya ujasiriamali.

Sambamba na hayo Mkuu wa Wilaya ametoa wito kwa makundi yote kushirikiana na serikali katika kuhakikisha wananchi wote wenye sifa wanajiandikisha na kutumia haki yao ya kupiga kura huku akiongeza kuwa ushiriki wao utasaidia kuimarisha demokrasia na kuchochea maendeleo endelevu katika wilaya ya Mvomero na nchini kwa ujumla.

Kwa upande wake Bw.  Thomas John kwa niaba ya waendesha boda boda wengine amemshukuru Mkuu huyo wa Wilaya na kuahidi kuwa watahakikisha kuwa wanahamasishana ili waweze kwenda kujiandikisha kwa ajili ya kuchagua viongozi bora wa Serikali za Mitaa.

Pamoja na mkutano huo, Mkuu wa Wilaya alianza kutoa hamasa hiyo ya kujiandikisha katika vitongoji vya KKKT, Kitolondo na Mnazi Mmoja.

"Serikali za Mitaa, Sauti za Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi".

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.