• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

CHANGAMOTO YA UHABA WA MAJI MANGAE YATATULIWA, WAZIRI MKUCHIKA ATOA NENO

Posted on: October 27th, 2024

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikuku (kazi Maalum) Captain Mstaafu Mhe. George Mkuchika (MB) ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwa usimamizi na ufuatiliaji mzuri wa fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo inawagusa Wananchi.

Mhe. Mkuchika amesema hayo Oktoba 27, 2024 wakati akizindua mradi wa maji Kata ya Mangae ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya siku moja Wilayani Mvomero ya kukagua, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mhe. Mkuchika ameeleza kuwa nia ya Serikali awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya maji hapa nchini ili kumtua mama ndoo kichwani huku akiwapongeza watendaji wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri wa fedha na kuweza kutekeleza miradi huo wa maji kwa kiwango cha juu.

"...Naishukuru Halmashauri kwa kusimamia vizuri matumizi ya fedha hizi hamkuruhusu mchwa kula noti za hapa..." amesema Mhe. George Mkuchika.

Awali, wakati akimkaribisha Waziri Mkuchika, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima  amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa niaba ya wananchi wa Mkoa huo kwa kuwajali na kuwaletea miradi mbalimbali hususan ya maji ambapo hapo awali kipindi cha kiangazi idadi kubwa ya mifugo hufariki kwa sababu ya uhaba wa maji ya kutosha.

Aidha, amesema uwekezaji huo wa tenki la maji katika kijiji cha Mangae  utaondoa changamoto  ya  upatikanaji wa maji huku akitumia fursa hiyo kumuomba Rais Samia kuendelea kutoa fedha ili kuweza kumaliza kabisa adha ya maji.

Naye, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mvomero Mhandisi Mlenge Nasib wakati akisoma taarifa ya mradi huo wa maji amesema mradi huo umegharimu jumla ya shilingi Milioni 643.7,  fedha zilizotumika ni shilingi Milioni 388.8  ambapo mradi huo umefikia asilimia 85% kukamilika huku akibainisha kuwa mradi huo utahudumia wakazi 4049 wa kijiji cha Mangae na maeneo jirani.

Nao wakazi wa kijiji hicho akiwemo Bi. Clinsensia Cosmasi amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaletea mradi huo wa maji ambapo hapo awali walikuwa wakichota maji kwenye mito ambayo siyo salama kwa afya zao lakink kupitia mradi wanaamini utakapokamilika utaenda kuondoa adha walizokumbana nazo kutokana na kutafuta maji.

Akiwa Wilayani Mvomero Mhe. Mkuchika ametembelea miradi mitano ya maendeleo ikiwemo ya Afya, Elimu na miundombinu ya Barabara.

MWISHO

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.