• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

CHANGAMOTO YA MAWASILIANO KIJIJI CHA MSOLOKELO KUWA HISTORIA

Posted on: December 3rd, 2024

Serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ipo mbioni kutekeleza ujenzi wa Mnara wa Mawasiliano katika Kijiji cha Msolokelo kilichopo Kata ya Pemba Wilayani Mvomero ili kuwaondolea adha wananchi wa eneo hilo ambao wamekuwa wakipata changamoto hiyo kwa muda mrefu.

Hayo yamebainishwa Disemba 03, mwaka huu na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Jerry Silaa akizungumza na wananchi wa kijiji hicho ikiwa ni ziara ya siku moja ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano Vijijini.

Waziri Silaa amesema kuwa Mnara huo ni miongoni mwa minara 14 inayojengwa Wilayani Mvomero ili kuhakikisha kuwa wananchi wanapata mawasiliano ya uhakika.

"...tumekwisha ongea na Vodacom kwa ajili ya ujenzi wa mnara wa Kijiji hiki cha Msolokelo..." amesema Mhe. Silaa.

Aidha, Waziri huyo amemuagiza Meneja wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Kanda ya Mashariki kushirikiana na Mbunge wa Mvomero Mhe. Jonas Van Zeeland pamoja na Viongozi wengine ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji kuhakiki maeneo mengine ambayo itajengwa minara hiyo 14ya mawasiliano ndani ya Wilaya hiyo.

Katika hatua nyingine Waziri Silaa amewataka wananchi wa kijiji cha Msolokelo na maeneo mengine ambako mradi wa minara 758 inajengwa kuwa wavumilivu na wenyesubira wakati Serikali ikiendelea kufanya kazi na kuhakikisha kuwa nia ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kufikisha mawasiliano kwa watanzania inafanikiwa.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe.  Jonas Van Zeeland akieleza changamoto ya mawasiliano katika Kata ya Pemba hususan kijiji cha Msolokelo amesema japokuwa kata hiyo ina mnara mmoja ambapo walitarajia mnara huo ungetatua changamoto ya mawasiliano ya kijiji hicho lakini kutokana na eneo hilo kuzungukwa na milima hivyo kijiji kinahitaji kuwa na mnara wake.

Ameongeza kuwa Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia mradi wa minara 758, jimbo la Mvomero limepata minara 14 lakini hadi sasa ni minara sita huku akibainisha kuwa sababu zinazotolewa na wataalam haziridhishi.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Mhandisi Peter Mwasalyanda wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa minara 758 amesema Mkoa wa Morogoro umepata minara 69 yenye thamani ya shilingi bilioni 11.17 ambayo inatekelezwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo. Hadi kufikia Disemba 02, 2024 jumla ya minara 19 tayari imekamilika na kuwashwa.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe. Yusuf Makunja amemshukuru Waziri Silaa kwa ziara hiyo yenye matumaini kwa wananchi wa Mvomero hususan katika upatikanaji wa mawasiliano ndani ya Halmashauri hiyo.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.