• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

BIMA YA AFYA KWA WOTE YAWAFIKIA WANANCHI MVOMERO, DC DOTTO AWAHIMIZA KUJIUNGA KWA GHARAMA YA TSH. 150,000

Posted on: January 30th, 2026

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Mhe. Maulid Dotto, amewahimiza wananchi wa wilaya hiyo kujiunga na Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ili waweze kupata huduma za afya kwa uhakika na kwa wakati akisema kuwa Serikali imeweka utaratibu rafiki unaomwezesha mwananchi kujiunga kwa gharama ya Shilingi 150,000 kwa mwaka kwa familia ya watu sita.

Mhe. Dotto ametoa wito huo Januari 30, 2026 wakatika akitoa salam za Wilaya kwenye kikao cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili taarifa za Robo ya Pili (Oktoba Disemba 2025), kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.

Mkuu wa Wilaya ameeleza kuwa utekelezaji wa mpango huo ni sehemu ya azma ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila kuachwa nyuma, huku akiongeza kuwa viongozi wa ngazi zote wanapaswa kuendelea kutoa elimu ili wananchi wajitokeze kujiunga.

“...mpango huu ni utekelezaji wa dira ya Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha huduma za Afya zinawafikia wananchi wote kwa usawa bila ubaguzi, ambapo kupitia mpango huu kaya italipa kiasi cha shilingi laki moja na elfu hamsini (150,000) kwa mwaka na bima hiyo itawahudumia watu sita kwa familia moja...” amesema Mhe. Dotto.

Aidha, ameongeza kuwa mpango huo ni utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote (Universal Insurance Act of 2023) ambao unalenga kuwasaidia wananchi wasio na uwezo wakiwemo Wazee, Watoto, Wajawazito na watu wenye ulemavu kupata matibabu kwa gharama zitakazotolewa na Serikali.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe. Koila Kurman Majuka amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa salam Pamoja na maelekezo aliyatoa hukua akimuhakikishia kuwa Waheshimiwa Madiwani kwa umoja wao watahamasisha wananchi kujiunga na mpango huo wa Bima ya Afya kwa Wote.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg. Paulo Faty amebainisha kuwa Halmashauri imejipanga kuhakikisha kuwa wananchi waliokusudiwa kujiunga na mpango huo wanajitokeza kwa wingi kwa kutoa hamasa ili lengo la Serikali la kuwapunguzia wananchi mzigo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI WILAYA (DCC)

    February 12, 2026
  • SERIKALI YACHUKUA HATUA KUTATUA MGOGORO WA ARDHI KIJIJI CHA DOMA, DC DOTTO ATAKA WANANCHI WALIO KATIKA ENEO LA MGOGORO KUTAMBULIWA

    February 11, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI LAPITISHA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI 2026/2027

    February 09, 2026
  • BIMA YA AFYA KWA WOTE YAWAFIKIA WANANCHI MVOMERO, DC DOTTO AWAHIMIZA KUJIUNGA KWA GHARAMA YA TSH. 150,000

    January 30, 2026
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.