• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

Posted on: April 13th, 2025

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Wilaya ya Mvomero imepongezwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 kwa kutekeleza miradi ya maji kwa ufanisi hivyo, kupunguza adha ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa Wilaya hiyo.


Pongezi hizo zimetolewa Aprili 13, 2025 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 Ndg. Ismail Ali Ussi wakati wa uzinduzi wa mradi wa usambazaji maji uliopo katika Kata ya Mangae.


Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amesema kuwa katika maeneo ambayo mwenge huo umepita umeshuhudia ufanisi mkubwa uliofanywa na RUWASA katika kutekeleza miradi yake kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.


Aidha, ameongeza kuwa ufanisi huo unajidhihirisha Wilayani Mvomero ambapo RUWASA imejenga mradi wa maji ambao ni mkombozi kwa wananchi wa Kata ya Mangae.


“...leo hii ndani ya Wilaya ya Mvomero inaonesha jitihada gani ambazo wanazifanya kama wenzetu katika kuwasaidia wananchi hongereni sana wenzetu wa RUWASA...” amesema Ndg. Ismail Ussi.


Sambamba na hilo Kiongozi huyo wa Mbio wa Uhuru amewasisitiza wananchi kutunza miundominu ya maji ili iendelee kudumu kwa muda mrefu na kuleta manufaa yaliyokusudiwa.


Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mvomero Mhe. Jonas Van Zeeland amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwatatulia kero ya maji wananchi wa Mangae ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta huduma ya maji safi na salama. Aidha, Mhe. Zeeland amebainisha kuwa miradi ya maji inayotekelezwa katika Wilaya hiyo inagharimu zaidi ya shilingi bilioni 15 huku akiongeza kuwa wahandisi wanaendelea na kazi.


Naye, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mvomero Mhandisi Mlenge Nasibu amesema mradi huo unagharimu kiasi cha shilingi milioni 643,750,000 chanzo cha fedha ni P4R yaani lipa kwa matokeo. Mhandisi Mlenge

ameongeza kuwa Manufa ya mradi huu ni kuondoa changamoto ya maji kwa wananchi wapatao 4049.


MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.