Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Morogoro katika kuhakikisha kwamba shughuli na fedha zote zinazoletwa na Serikali zinasimamiwa na kutumika kutokana na miongozo. Na hivi leo ameifikia Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.
Ziara hiyo imemfikisha katika Hospitali ya Wilaya hiyo ambapo baada ya kufanya ukaguzi, amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kuhakikisha anamaliza changamoto za hospitali hiyo haraka iwezekanavyo kwa lengo la kuwasaidia Wananchi wa Mvomero pia kupata huduma za afya karibu na meneo yao na kumuelekeza Mganga Mkuu wa Wil;aya hiyo awajulishe wananchi juu ya huduma za afya zinazo patika katika Hospitali yao ya Wilaya .
Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo katika ziara yake ya kikazi ya kukagua Miradi ya kimkakati akiambatana na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Rebecca Nsemwa ,Mkurugenzi Mtendaji Mwl .Linno Mwageni na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe .Yusuph Makunja.
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.