• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

RAIS SAMIA AZINDUA KAMPENI YA TUTUNZANE MVOMERO, ASEMA NI MFANO WA KUIGWA NCHINI

Posted on: August 3rd, 2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Kampeni ya Tutunzane Mvomero leo Agosti 3, 2024 huku akisema  kuwa ni ya mfano hapa nchini katika kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji.

Akizungumza wakati akizindua kampeni hiyo Dkt. Samia Suluhu Hassan  amewapongeza viongozi wa Mkoa na Wilaya pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwa na mpango madhubuti wenye dhamira ya kudumisha amani kwa kuepusha migogoro ya wakulima na wafugaji ndani ya Mkoa wa Morogoro na Taifa kwa Ujumla huku akibainisha kuwa mradi huo ni wa mfano kwenye maeneo yote yenye migogoro.

"...Serikali inaunga mkono Kampeni hii ambayo inaweza kuwa ya mfano kote nchini..." amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia  amebainisha umuhimu wa kampeni hiyo ambapo amesema mradi huo unaenda kuepusha migogoro na kudumisha amani kwenye maeneo husika, kuwezesha ufugaji wa kisasa, kuwawezesha wakulima kuongeza tija ya uzalishaji, mradi utasaidia wakulima na wafugaji kukopesheka kupitia hatimiliki zao pia mradi huo utasaidia utunzaji wa mazingira.

Sambamba na hilo, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kuweka msukumo katika kuboresha Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa kuwa sekta hizo zina fursa nyingi na zimeajiri watu wengi zaidi.

Naye, Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa jitihada alizozifanya juu ya kampeni hiyo ambayo imewezesha watu 1066 kujiunga katika kampeni hiyo. Aidha, amebainisha kuwa Serikali imetenga kiasi cha milion 70 kwa ajili ya uchimbaji wa visima 60 Wilayani Mvomero. Ameongeza kuwa Msimu ujao wa Kilimo Wizara italeta tani 50 ambazo zitawasaidia wakulima waishio karibu na hifadhi ya Mikumi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru Rais Samia kwa kuzindua kampeni hiyo ya tutunzane ambayo inaenda kuwa chachu ya utatuzi wa migogoro ya wakulima na wafugaji katika Mkoa huo pia amesema kampeni hiyo itatumika katika wilaya zote ambazo zinachangamoto ya wakulima na wafugaji.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO YAWEKA MIKAKATI YA KUFANYA VIZURI KATIKA KIPENGERE CHA USAFI WA MAZINGIRA

    August 20, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU ZA UTEUZI LAENDELEA KUSHIKA KASI

    August 20, 2025
  • UTOAJI WA FOMU ZA UTEUZI

    August 19, 2025
  • DC MAULID DOTTO AAHIDI KUTAFUTA ENEO KWA AJILI YA MASHINDANO YA MAGARI

    August 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.