Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 Ndg. Godfrey Eliakimu Mzava ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kwa kuwarithisha watoto elimu ya utunzaji wa mazingira ili waweze kuwa mabalozi wazuri katika jamii juu ya utunzaji wa mazingira ambapo imeelezwa kuwa Wilaya hiyo imeanzisha klabu 57 zinazotoa elimu ya utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi wa shule za awali na msingi.
Ndg. Godfrey Mzava ametopongezi hizo Aprili 20, 2024 wakati mwenge wa Uhuru ulipotembelea shule ya Msingi Manyinga kwa ajili ya kukagua na kuona maendeleo ya mradi wa utoaji elimu ya utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi wa shule za awali na msingi shuleni hapo.
Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amesema watoto wakipatiwa elimu ya utunzaji wa mazingira itaisaidia jamii kuwa na mabalozi wazuri na wazalendo katika kutunza mazingira kwa vizazi vya sasa na baadaye.
“…ukiendelea kuwalea watoto hawa wadogo wakatambua umuhimu wa uhifadhi wa mazingira watakuja kuwa watu wakubwa na watakuwa mabingwa wazuri sana wa masuala ya utunzaji wa mazingira…”amesema Ndg. Godfrey Mzava.
Aidha, ameongeza kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazopata athari za mabadiliko ya tabia ya nchi yanayotokana na shughuli zisizofuata uendelezaji na utunzaji wa mazingira zikiwemo uchomaji wa misitu, kilimo, ufugaji, kilimo na shughuli kama za viwandani.
Nao wanafunzi waliopata elimu ya utunzaji wa mazingira shuleni hapo akiwemo Jackline Eliaba mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Manyinga amesema suala la upansaji miti ni la kila jinsia yaani wanawake kwa wanaume huku akibainisha kuwa ushiriki wa jinsia zote katika upandaji miti na usafi wa mazingira utasidia kukakabiliana na athari za mabadiliko ya tabia ya nchi.
Kwa upande wake Jenifa Solomon mwanafunzi wa darasa la saba katika shule hiyo amebainisha kuwa shule hiyo ni miongoni mwa shule 57 zinazotoa elimu ya utunzaji wa mazingira Wilayani humo. Aidha, kwa niaba ya wanamazingira wa Wilaya hiyo amewaomba wananchi Wilayani humo kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika hapa nchini mwezi Oktoba, 2024.
Mwenge wa uhuru umemeliza mbio zake Wilayani Mvomero ambapo umekagua, kuona, kuzindua na kuweka mawe ya msingi miradi nane yenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 1.4.
MWISHO.
Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero
Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO
Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348
Mobile: +255 23 293 4348
Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz
Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.