• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MRADI WA SAUTI ZETU KUWAWEZESHA WENYE ULEMAVU KUPATA HAKI ZA MSINGI

Posted on: November 26th, 2024

Mradi wa Sauti Zetu unaotekelezwa na Shirika la SAWA Wanawake Tanzania unalenga kuwakomboa watu wenye ulemavu hususan katika upatikanaji wa haki za msingi ikiwa ni pamoja na elimu, afya, ajira, na ushirikishwaji katika maamuzi ya kijamii.

Hayo yamebainishwa Novemba 26, 2024 na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Dkt. Phillipina Phillipo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, wakati akifungua kikao kazi cha wadau wa elimu jumuishi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Akizungumza katika kikao hicho Dkt. Philippina ameshukuru Shirika la SAWA kwa kuja na mradi huo wa Sauti Zetu ambao unalenga kuvunja vikwazo vya kijamii na kiuchumi vinavyowakumba watu wenye ulemavu kwa kuwapatia fursa na zana za kujisimamia.

Aidha, amesema kumekuwa na changamoto katika jamii kwamba baadhi ya wazazi hawatoi taarifa za uwepo wa watu wenye ulemavu katika familia zao badala yake wanawafungia ndani na kuwanyima haki zao ikiwemo ya kupata elimu na huduma za afya, huku akibainisha kuwa mradi huo utasaidia jamii ya wanamvomero kutoa taarifa za walemavu ili wanufaike na fursa mbalimbali.

“...kwanza nishukuru hili suala wa sababu tunajua ni changamoto ambayo ipo kila sehem...kupitia huu mradi wananchi tutahamasika na tutakuwa tupo tayari kuhusiana na watu wenye ulemavu..." amesema Dkt. Phillipina.

Sambamba na hilo, Dkt. Phillipina amebainisha mipango ya Serikali ambayo inawagusa watu wenye ulemavu ikiwemo ujenzi wa miundombinu kama vile vyoo maalum kwa ajili ya wenye ulemavu kwenye shule na vituo vya Afya pamoja na Serikali pia inatoa mikopo ya asilimia 10 ambayo hutolewa na Halmashauri ambapo asilimia 2 ni kwa ajili ya kundi hilo.

Naye, Bw. Mahamud Ngamungi ambaye ni Afisa Ubora wa Elimu kutoka shirika la SAWA Wanawake Tanzania amesema kikao hicho kimewakutanisha wadau wa elimu jumuishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero ambao walishiriki zoezi la ufuatiliaji wa utekelezaji wa mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi ambao ulianza mwaka 2021 na utaisha mwaka 2026. Ameongeza kuwa mradi wa Sauti Zetu unamaanisha ni sauti za wanafunzi wenye mahitaji maalum ambapo mahitaji hayo yanahitaji kuzingatiwa ili waweze kupata elimu bora.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Msingi Msasani Mwl. Immanuel Kahaya amelishukuru Shirika la SAWA kupitia mradi wa Sauti Zetu ambapo mradi huo sio tu kuwapatia elimu bali umechangia kuboresha miundombinu ya wanafunzi wenye ulemavu katika shule hiyo, huku akiishukuru Serikali kwa kutoa fedha za chakula kila mwezi kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MVOMERO KUENDELEZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO KUPITIA GoT-HoMIS KWENYE VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA

    May 09, 2025
  • MOROGORO YAJA NA MKAKATI KUSHUGHULIKIA MADAI YA WAFANYAKAZI

    May 01, 2025
  • DC NGULI ATIMIZA AHADI YA KUGHARAMIA MATIBABU YA KIJANA RAMADHANI MOHAMED

    April 28, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUWAPUUZA WANAOCHOCHEA UVUNJIFU WA AMANI

    April 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.