• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

MMILIKI WA MGODI WA DHAHABU DOMA APEWA SIKU TATU KUKAMILISHA MIUNDOMBINU MUHIMU MGODINI

Posted on: January 27th, 2025

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Mvomero imeagiza mmiliki wa mgodi wa dhahabu uliopo katika Kata ya Doma kukamilisha miundombinu muhimu mgodini ndani ya siku tatu, agizo hilo limetokana na ukaguzi uliofanywa na maafisa wa madini na kugundua mapungufu yanayoweza kuhatarisha usalama wa wafanyakazi na mazingira.

Agizo hilo limetolewa Januari 27, 2025 na Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli alipotembelea mgodini hapo na kujionea hali ya usalama na miundombinu duni inayohatarisha maisha ya wachimbaji na kutoa maelekezo kwa mmiliki wa mgodi huo.

"...sasa leo tutakagua hapa na tutamtaka mwenye eneo hili aweke miundombinu hiyo haraka ndani ya siku tatu tukute hivyo vitu viko tayari...usilale usiku na mchana vinginevyo tutafunga huu mgodi...” amesema Mkuu wa Wilaya.

Aidha, Mhe. Nguli amewataka wachimbaji katika mgodi huo kujilinda dhidi ya wanyama wakali kama simba na tembo kwani eneo hilo lipo karibia na hifadhi. Pia, amesisitiza umuhimu wa kulinda mazingira kwa kuhakikisha taka zote zinahifadhiwa vizuri.

Naye, Afisa Madini Mkazi, Mkoa wa Morogoro Bi. Zabibu Napacho amesema mmiliki wa eneo hilo ambalo lina leseni alitoa taarifa kwenye ofisi hiyo kufuatia kuvamiwa na wachimbaji wadogo waliotoka katika maeneo mbalimbali huku akimshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kutembelea eneo hilo ili kuhakikisha kuwa wachimbaji hao wanafuata sheria za madini.

Kwa upande wake Mhifadhi Wanyamapori Msaidizi Kata ya Doma Simon Ibrahim ametoa wito kwa wachimbaji wa eneo hilo kuchukua tahadhari zaidi juu ya wanyama hatarishi wakiwemo tembo na simba ili waendelee kuwa salama na kuendelea kujitafutia riziki.

Bw. Amini Membe ambaye ni mmiliki wa mgodi huo ameahidi kufanyia kazi maagizo hayo kwa haraka na kuimarisha usalama wa mgodi. Akizungumzia suala la mapato ya kijiji amesema atahakikisha kijiji kinapata mapato yake kama inavyotakiwa.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RUWASA MVOMERO YAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI KWA UFANISI

    April 13, 2025
  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.