• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DED MVOMERO APONGEZA MRADI WA BASIN, ATAKA JAMII ISHIRIKISHWE KULETA MATOKEO CHANYA

Posted on: September 10th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Ndg. Paulo Faty amepongeza jitihada zinazotekelezwa kupitia Mradi wa Behavioural Adaption for Water Security and Inclusion (BASIN) uliopo chini ya Shirika la Shahidi wa Maji kwa lengo la kupunguza athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi huku akisisitiza kuwa ushirikishwaji wa jamii ni nguzo muhimu katika kufanikisha matokeo chanya ya mradi huo.


Ndg. Faty ametoa wito huo Septemba 10, 2025 wakati akifungua Warsha ya mafunzo kwa Viongozi na Wataalam kuhusu taarifa za Tahadhari ya mapema ili kukabiliana na majanga ya hali ya hewa yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi, warsha hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.


Akizungumza katika warsha hiyo, Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa Shirika la Shahidi wa Maji pamoja na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ni wadau muhimu katika Wilaya ya Mvomero, akiongeza kuwa taarifa za tahadhari za mapema zina mchango katika uzalishaji wa mazao ya kilimo pamoja na malisho ya mifugo.


Aidha, amesisitiza kuwa kuna umuhimu wa kuweka mikakati ya kuishirikisha jamii ipasavyo kwa kuwa ndiyo waathirika wa moja kwa moja kutokana na mabadiliko ya tabianchi.


“...tuweke mikakati mizuri ni namna gani tutashirikisha jamii zetu, waweze kufahamu ni nini cha kufanya ni kilimo gani sahihi kwa mazingira, matumizi bora ya maji...” amesema Ndg. Paulo Faty.


Ameongeza kuwa Halmashauri itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu kwa wadau wanaosimamia mradi huo ili kuhakikisha rasilimali zinazotolewa zinatumika ipasavyo na kila mwananchi ananufaika.


Kwa upande wake Mratibu wa Utafiti kutoka Shirika la Shahidi wa Maji Bw. Vitus Tondelo amesema kuwa Shirika hilo linajikita katika kutafiti, kuibua na kutoa suluhisho kwa changamoto zinazoikumba sekta ya maji. Aidha, amesema Mradi wa BASIN unahakikisha kuwa tabia za mwanadam zinabadilika ili kuleta uhimilivu mabadiliko ya tabianchi katika upatikanaji wa uhakika wa maji. Mradi huo unatekelezwa katika nchi tatu za Tanzania, Malawi na Bukinafaso, kwa Mvomero mradi unatekelezwa Vijiji vya Kambala, Mkindo, Vikenge na Kinda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 14, 2025
  • MAJINA YA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WALIOITWA KWENYE USAILI OKTOBA 17, 2025 October 14, 2025
  • MAJINA YA RESERVE WA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANAOTAKIWA KWENYE USAILI KATIKA KATA October 14, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DKT. BASHIRU AIPONGEZA KAMPENI YA TUTUNZANE MVOMERO, ATAKA IWE NYENZO KUHAMASISHA UZALISHAJI MALISHO, UPATIKANAJI WA MAJI

    November 26, 2025
  • DC MAULID DOTTO ALETA TABASAMU KWA KIJANA KIDARIS BABO, AMKABIDHI KITI MWENDO KUMUWEZESHA KUTEMBEA

    November 21, 2025
  • WASIMAMIZI, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO KUHAKIKISHA UCHAGUZI UNAKUWA WA HURU NA HAKI

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI, WASIMAMIZI WASAIDIZI VITUO VYA KUPIGIA KURA WATAKIWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA UADILIFU, UAMINIFU NA UZALENDO

    October 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.