• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
MVOMERO DISTRICT COUNCIL
MVOMERO DISTRICT COUNCIL

Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Halmashauri
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Uongozi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
    • Baraza la Madiwani
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Rasilimali Watu
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Itakayo tekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
    • Viwanda
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti

DC NGULI AWATAHADHARISHA WANUNUZI WA ARDHI WILAYANI MVOMERO AWATAKA KUFUATA UTARATIBU

Posted on: January 30th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Judith Nguli, amewataka wananchi wanaotaka kununua ardhi kufuata taratibu zote za kisheria ili kuepuka migogoro na hasara zinazoweza kujitokeza.

Mhe. Nguli ameyasema hayo Januari 30, 2025 wakati akifunga mafunzo elekezi kwa Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji pamoja na Watendaji wa Vijiji yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Mzumbe.

Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha kuwa kumekuwa na ongezeko la malalamiko kuhusu watu kununua ardhi kiholela bila kufuata utaratibu, jambo linalosababisha migogoro ya mara kwa mara huku baadhi ya Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na watendaji wakitajwa kuwa sehemu ya migogoro hiyo.

“…nitoe agizo kwa wananchi wanao nunua ardhi, kwa mihuri ya mwenyekiti, mtendaji na serikali yake haifanyi wao kuwa halali kumiliki ardhi, hiyo ni batiri, taratibu za uchukuaji ardhi zinajulikana…” amesema Mkuu wa Wilaya.

Ameongeza kwa kuwataka wenyeviti hao kuhakikisha kuwa wanafuata taratibu za kumilikisha ardhi ya kijiji ikiwa ni pamoja na ridhaa ya mkutano mkuu wa kijiji ambao ndiyo wenye mamlaka ya kudhiria mwanchi kupatiwa ardhi.

Pamoja na hayo, Mhe. Nguli amewataka wenyeviti hao kudhibiti migogoro kwenye maeneo yao ikiwemo migogoro ya ardhi na migogoro ya wakulima na wafugaji ili kuhakikisha kuwa Amani na utulivu vinaendelea kudumishwa katika wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Afisa Utumishi wa Halamshauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Stephen Mmanywa amesema lengo ni kuhakikisha kuwa wenyeviti hao wanakwenda kutekeleza majukumu yao kwa usahihi huku akitaja mada zilizofundishwa na wawezeshaji ikiwemo, matumizi bora ya ardhi, sheria za mamlaka za serikali za mitaa,  fedha na manunuzi. Pia, Bw. Mmanywa ameeleza kuwa matarajio yao baada ya mafunzo hayo ni uwepo wa utawala bora pamoja na kuondoa migogoro ya ardhi na changamoto nyingine za wananchi wa wilaya hiyo.

Naye Bi. Scholastica Nyabweke ambaye ni mwezeshaji wa mafunzo hayo kutoka chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo amewapongeza wenyeviti hao kwa mafunzo hayo huku akiwasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya serikali.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wenyeviti hao, Mhe. Ally Masalika ambaye ni mwenyekiti wa Kitongoji cha Kiwanjani, amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa hotuba nzuri huku akiwashukuru wawezeshaji kwa mada nzuri, pia ametumia fursa hiyo kuwasisita wenyeviti kwenda kuyafanyia kazi mafunzo kwa vitendo katika maeneo yao ili yalete tija.

MWISHO.

Matangazo

  • MAJINA YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR KIT OPERATORS. February 22, 2025
  • Majina ya Waandishi wasaidizi na BVR KIT Operators February 22, 2025
  • Kuitwa Kwenye Usahili Nafasi Ya Mtendaji Wa Kijiji,Mtunza Kumbukumbu,Afisa Hesabu Msaidizi,Dereva wa Ambulance na Katibu Muhtasi. October 12, 2021
  • TENDER MVOMERO May 28, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU KUMULIKA MIRADI YA MAENDELEO 7 YENYE THAMANI YA TSH. 1.06 WILAYANI MVOMRO

    April 13, 2025
  • DC MVOMERO AAGIZA SHULE SHIKIZI MINGO ISAJILIWE, IPOKEE WANAFUNZI JANUARI 2025

    March 27, 2025
  • KUU MVOMERO YAKISHUKURU KIWANDA CHA SUKARI MTIBWA KWA KUSAIDIA WANANCHI KURUDISHA MTO KWENYE MKONDO WAKE

    March 19, 2025
  • RAS MOROGORO AENDELEZA KAMPENI YA "JISOMESHE NA MKARAFUU" KUWAWEZESHA WANAFUNZI KIUCHUMI

    March 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani kimkoa yafanyika Halimashauri ya Wilaya Mvomero
Video Zaidi

Viungo vya Haraka

  • Ukurasa wa Facebook

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira
  • Baraza la Mtihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Wami Sokoine, Dakawa, Mvomero

    Anwani Ya Posta: P.O BOX 663, MOROGORO

    Msaada wa Kiufundi: +255 23 293 4348

    Mobile: +255 23 293 4348

    Baruapepe: ded@mvomerodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani Eneo
    • Huduma

Hakimiliki ©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero.Haki zote zimehifadhiwa.